Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nikushukuru kwa kuniona. Kutokana na muda nianze moja kwa moja na ku-declare interest kwamba mimi ni mjumbe wa Kamati ya Sheria Ndogo. Katika mijadala yetu ndani ya Kamati, ndiyo maana nimekaa upande huu ili niwaone vizuri Mawaziri kwa hili jambo ninalotaka kulisema ni kwamba Mawaziri wangu na Idara ya Uandishi wa Sheria Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe kuna tatizo. Sheria nyingi zinakuja haziko tayari na reference zinazofanyika siyo sahihi. Mheshimiwa Mwenyekiti, utakuta reference ya Sheria ya Mifugo lakini ukirudi kwenye Sheria Mama unaona ni Sheria Inayozuia Vyombo Vinavyokwenda Mwendokasi. Sasa hili si jambo zuri na wewe ni mwalimu wangu na mimi nakuheshimu sana. Hili jambo napenda kidogo tuwe makini, kwa sababu sheria hizi zinaweza kuwa katika karatasi lakini unapokwenda kuzifanyia kazi ndipo matatizo yanapoanza. Sasa tungependa jambo hili nalo tuliweke vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nieleze masikitiko yangu niliposikia wakati Mheshimiwa Adadi anatoa ripoti yake kwamba nchi yetu haina Sera ya Ulinzi. Hili ni jambo la kusikitisha. Nchi yetu ni moja ya nchi ambayo inasifika sana kwa maana vyombo vyetu vya ulinzi na usalama viko mstari wa mbele, tuna jeshi ambalo limekuwa credited kwamba ni moja ya majeshi 10 bora duniani sasa.
Kama tena jeshi letu zuri, lenye sifa, lakini sera ya ulinzi haipo tayari, tunaweza tukaingia katika matatizo makubwa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana katika jambo hili, mara kwa mara tumekuwa tunalalmika sisi Wabunge hasa mimi binafsi nikieleza juu ya matatizo yanayotokea katika eneo la Kibindu, Mvomero, Kwekonje na Kimange kwamba watu wanauana lakini majeshi yetu hayachukui hatua. Tusije kufikia sehemu tukaamini kwamba kumbe kwa sababu ya kukosekana kwa sera zinazotoa uelekeo wa jinsi ya kujipanga vizuri juu ya ulinzi ndiyo maana wananchi wangu wa Halmashauri na Jimbo la Chalinze wanaendelea kufa kwa sababu hakuna hatua zozote ambazo zinachukuliwa. Naomba sana jambo hili Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi ilifanyie kazi ili sera hii ije mapema iwezekanavyo ili tuweze kupanga nchi yetu vizuri kwa faida ya leo, kesho na kesho kutwa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyeiti, pamoja na hilo napenda nizungumzie suala la madeni kwenye vyombo vyetu. Nimesoma kwenye taarifa na nimesikiliza Mheshimiwa Adadi akiwa anatoa taarifa yake, vyombo vyetu vinadaiwa sana. Hebu sasa Serikali tujipange tumalize madeni haya kwa sababu itafika sehemu vyombo vyetu vitakuwa havikopesheki wala kupatiwa vifaa vya kisasa kwa sababu ya uzito wa kulipwa kwa madeni hayo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Mkuchika, Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Maadili kwa taarifa yake nzuri ambayo imeeleza jinsi walivyojadili masuala mbalimbali yaliyoifikia Kamati. Hata hivyo, jambo moja ambalo napenda niwaeleze wenzangu na hasa Mwenyekiti wetu ni kwamba mimi walionifundisha maisha walinifundisha kujiheshimu kwanza kabla wenzako hawajakuheshimu. Mheshimiwa Mwenyekiti, tusipofanya hivyo ama tusipokuwa na philosophy ya namna hiyo kila siku kazi yetu itakuwa ni kupigishana makelele kama ambavyo unaona leo hii Wabunge wanasema ya kwao, huko Serikali inasema ya kwake, kunaonekana kama kuna mgogoro baina ya makundi haya mawili jambo ambalo linahatarisha hata usalama wa Taifa letu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa uliniambia unanipa dakika tano nisingependa kuzama sana kwenye mambo mengine niwaachie wenzangu nao waendelee kuchangia. Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante sana.