Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami naomba nichangie kwenye Kamati hii ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na suala zima la tozo ile ya fire. Tunapolipia road licence kuna shilingi karibia Sh.30,000 mpaka Sh.40,000 zinakwenda kwenye huduma za zimamoto kwa maana ya fire. Sasa nataka kujua kupitia Kamati na Wizara kwamba pesa hizi zinatumika katika eneo gani? Kwa sababu huduma za zimamoto katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Tanga na Mbeya bado tunaona wanatumia magari ambayo hayana uwezo wa kutoa huduma hii katika maghorofa marefu zaidi. Mheshimiwa Mwenyekiti, ni matarajio yangu kwamba kwa sababu pesa hizi zinakusanywa kupitia TRA na zina uhakika wa kupatikana sasa zingekwenda kuboresha huduma ya hivi vyombo vya kuzimia moto katika manispaa zote ili angalau tuwe na vyombo vya zimamoto vya kisasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo kwa Jiji la Dar es Salaam ambalo sasa hivi tuna huduma ya mabasi yaendayo kasi, ni kweli tumeingia katika dunia ya ushindani wa teknolojia lakini gari hizi zinazobeba magari yaliyoharibika kwa maana ya breakdown bado wanaendelea kutumia land rover ambazo mara nyingi zinasababisha kuharibu zaidi hata hayo magari. Kwa sababu siyo magari yote yanayovutwa na breakdown ni mabovu, mengine labda wame-pack katika maeneo ambayo sio sahihi, kwa hiyo wakati wanayavuta haya magari wanasababisha uharibifu kwa magari yanayovutwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwombe Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Mambo ya Ndani kwamba yeye ni kijana wa kisasa hebu alete huu usasa katika hizi breakdown tupate ambazo zinaendana na wakati tuliokuwa nao. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nizungumzie suala zima la ulinzi na usalama hasa katika Mkoa wetu wa Tanga ambapo tulikumbwa na tukio moja ambalo lina harufu ya ugaidi. Mwezi wa Nane na wa Tisa yalitokea mapigano, watu wenye silaha walivamia baadhi ya vijiji katika Jimbo la Mlalo na Lushoto wakafikia hatua wakachoma bweni la Chuo cha SEKOMU. Kwa hiyo, ni rai yangu kwamba kwa kuwa Mkoa wa Tanga uko pembezoni mwa nchi jirani ya Kenya na tunajua kabisa kwa kule upande wa Kenya kuna tishio la Al-shabaab, basi nataraji kwamba zile harufu lazima zitakuwa zinapenya katika maeneo yetu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia wapo askari hodari ambao wameweza kupambana katika tukio hili, kuna Inspector Joram ambaye mara ya mwisho alifanikiwa kukamata magaidi wawili wa Kisomali katika hilo kundi na hawa ndiyo waliokwenda kuonesha silaha zaidi ya tisa zilizokuwa zimefichwa kwenye kaburi na wakasaidia angalau kuufuatilia ule mtandao. Nitoe rai kwa Waziri mwenye dhamana awaone hawa vijana ambao wanafanya kazi nzuri waweze kupongezwa kwa sababu kazi waliyofanya ni kazi ya kishujaa na kizalendo. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwa upande wa magereza tunalo gereza kongwe sana linaitwa Gereza la Kilimo la Mngalo, ni miongoni mwa magereza ya mwanzo kabisa yanayojishughulisha na kilimo. Hata hivyo, gereza hili linatumika chini ya kiwango kwa sababu lina uwezo wa kubeba wafungwa 100 lakini wapo 38. Niombe kule kwenye msongamano ikiwemo Rorya, Tarime na kwingineko basi unaweza ukawasogeza huku Mlalo waweze kutusaidia katika shughuli za kilimo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.