Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii lakini hujaniambia nitachangia dakika ngapi? MWENYEKITI: Dakika tano tu. MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia Kamati hii ya Mambo ya Ulinzi na Usalama. Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nijikite sana katika masuala ya kuchukua vijana wa JKT hasa kwa upande wa Zanzibar. Kuchukua vijana wa JKT kwa upande wa Zanzibar ni suala zuri sana, lakini kutokana na utaratibu ambao unachukuliwa hawa vijana siyo utaratibu ambao unaridhisha. Kupitishia vijana kwa Wakuu wetu wa Mikoa kwa upande wa Zanzibar ni tatizo sugu sana. Kule Zanzibar tuna Kikosi cha JKU ambacho kikosi hiki kinafanana na Kikosi cha JKT kina mahusiano mazuri na Kikosi hiki cha JKT. Namuomba Mheshimiwa Waziri Ndugu yangu Dkt. Hussein Mwinyi akubaliane na masuala haya tuhakikishe vijana wanaochukuliwa kwa upande wa Zanzibar kuja katika Kikosi cha JKT wapitie katika kikosi hiki cha JKU, ninaamini tutapata vijana wazuri ambao ni wasikivu na imara ambao tunawataka. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri nikuombe sana hata bajeti nilichangia suala hili tuwaongeze vijana katika upande wa Zanzibar; vijana wanaotakiwa kuchukuliwa kwa upande wa Zanzibar angalau tufikishe asilimia kumi. Katika vijana 5,000 ambao wanatakiwa kuchukuliwa katika Jeshi la JKT angalau vijana 500 watoke upande wa Zanzibar, tupunguze msongamano wa ajira kwa upande wa Zanzibar. Nikuombe sana Mheshimiwa Waziri kwa kuwa katika bajeti yako ambayo umezungumza fedha zako hazitoshi, lakini uwezo wa kuchukua vijana hawa unao. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe sana Serikali itusaidie sana kwa upande wa wizara hii iwaongezee bajeti ya fedha ili waweze kuchukua vijana wengi kupunguza msongamano wa vijana katika jamii zetu. Nikuombe sana na tuiombe Serikali itusaidie juu ya hili kwa kuwa Mheshimiwa Waziri anasema nafasi anayo kubwa ya kuchukua vijana na anao uwezo mkubwa lakini tatizo ni fedha kidogo. Tumuombe Waziri wa Fedha akija na bajeti aweze kutusaidia atuongezee bajeti ili tuweze kumpa nafasi Mheshimiwa Waziri aweze kuchukua vijana wengi kwenda katika Jeshi la JKT. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie na suala la Wizara ya Mambo ya Ndani. Wizara ya Mambo ya Ndani inafanya kazi zake vizuri lakini vilevile tatizo ni fedha. Hawa askari wetu wanaishi maisha duni ambayo hata hayahesabiki, wanakaa katika makazi mabovu suala hili Mheshimiwa Waziri tunalizungumza kila siku ndani ya Bunge hili halijapatiwa ufumbuzi. Hebu leo nataka ukija utueleze hapo mbele, hivi nyumba za hawa askari ni lini utaanza kuzijenga? Isiwe kila siku maneno tu hapa katika Bunge lako hili. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia suala la fedha kwa Wakuu wa Vituo vyetu hawa wanahudumia mahabusu wao wenyewe, kuwalisha wao wenyewe na hata umeme ndani ya vituo vyetu hivi vya polisi wanatoa wenyewe Wakuu wa Vituo. Ukiangalia kiukweli hii kadhaa kubwa katika nchi yetu. Ni aibu Mkuu wa Kituo mshahara wake tunaujua basi anaendelea kuwalisha mahabusu kwa nguvu zake yeye mwenyewe. Tunakwenda wapi katika Wizara hii? Tukigusa makazi mabovu, uendeshaji mbovu na ndani ya vituo vyetu magari hatuna na nyumba za askari mbovu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kama pale Ziwani wakati mmoja nilienda kutembelea pale Ziwani tumekuta nyumba za askari zinashangaza sana nyumba hizi na ni hatari kubwa. Mtu anaingia kwa kuinama, kama hakuna uwezo wa kuzitengeneza nyumba hizi basi hata marekebisho ya kuzifanyia repair hizi nyumba upatikane….
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe sana, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.