Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. CAN.RTD Ali Khamis Masoud

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mfenesini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. KANALI (MST.) MASOUD ALI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi ya kuchangia machache katika Kamati yetu hii. Mimi mwenyewe ni Mjumbe wa Kamati hii ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Mapendekezo mengi tumeyatoa, lakini yapo mambo yanatukwamisha sisi wenyewe kwa kutokuwa watekelezaji wazuri wa majukumu yetu. Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ambalo tumeliona katika magereza yetu, mimi mwenyewe nilipata nafasi ya kutembelea magereza mengi hapa nchini lakini ninayoyakuta huko nashangaa kwa nini tunashindwa kuyasimamia. Wabunge wengi wanasimama hapa wanasema magereza wana maeneo makubwa ya kilimo na magereza wanaweza wakajiwezesha. Wanayo maeneo ya kilimo, tunawasaidiaje kuweza kuyalima hayo maeneo? Hilo ndiyo tatizo. Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Songwe mfano, wanasema wao wanaomba matrekta kwa ajili ya kufanyia kazi na mimi kwa mara ya kwanza toka nimezaliwa sijawahi kumuona mfungwa anaomba pembejeo, mfungwa analalamika hatuletewi pembejeo, hatuletewi matrekta, kumbe watu wanataka kufanyakazi lakini sisi wenyewe tunashindwa kuwawezesha. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, wanakwambia wanadai pesa nyingi ambazo hata hayo matrekta wangeweza kujinunulia, wanajilisha wenyewe, wanajitosheleza kwa chakula na wanalisha na magereza nyingine lakini bado tunashindwa kuwawezesha kuwapa vifaa vya kuongeza kilimo. Mimi nilikuwa naomba sana tuliangalie hili na ikiwezekana tuwapatie uwezo wa kukopeshwa hayo matrekta kama upo uwezo ili wafanyekazi watuzalishie na inawezekana wakaweza kulisha magereza mengi zaidi hapa nchini. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine nilikuta pia gereza moja hapa Morogoro; ni gereza linazalisha maziwa kwa wingi tu, lakini wanakwambia gari la kupelekea maziwa sokoni hawana. Sasa tufanyeje tuwaache wenyewe wanywe maziwa au tufanye nini? Lakini cha msingi kama kweli wanazalisha, wana uwezo mkubwa kwa nini tusiwapatie hata gari la kupeleka maziwa sokoni? Halafu ukiwauliza wanakwambia kwenye akaunti yao wanazo milioni 40; kwa nini hamnunui wanasema aah, utaratibu hauturuhusu. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi sielewi mtu anakuzalishia, anakupatia pesa, lakini wewe kumuwezesha ili azidishe kuzalisha huwezi, mambo mengine haya hayataki kusoma shule wala wapi. Tukae kitako tu tuamue ili wenzetu hawa wapate kuzalisha na waweze kusaidia magereza mengine. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka niliongezee hapa kuna hawa wafungwa waliohukumiwa kunyongwa; wameshahukumiwa wale wanasema, mimi nimeshawatembelea nimezungumza nao na ni hatari kuzungumza na watu wale, lakini tumezungumza nao maana wamekaa mia mbili, mia tatu kama hivi wakikutizama unaweza ukachanganyikiwa. Wanasema haki yetu tuliyoipata mahakamani ni kunyongwa, sasa kwa nini hatunyongwi? Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunaona maana kuna viongozi wengine hapa tunatunga sheria, tunatakiwa tuzitekeleze lakini tunaogopa dhambi. Sasa kama lengo ni kuogopa dhambi kwamba hatuwezi kunyonga basi sheria ibadilishwe, lakini kama sheria imewekwa inatakiwa itekelezwe basi kila mtu atekeleze. Tunahimiza kila siku kila mtu atekeleze wajibu wake, kama hukumu ya kunyongwa imetolewa na hatuwezi kunyonga tubadili sheria au kama tunaweza kunyonga basi tunyonge maana wale wanadai haki yao na haki yao ni kunyongwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nilitaka kulizungumza hapa lililonisikitisha sana zaidi kule Mbeya; tumekwenda tunaambiwa kule hakuna gari la Zimamoto lakini tunaambiwa ikitokea tatizo la moto gari lazima litokee uwanja wa ndege. Sasa hebu tujiulizeni Waheshimiwa Wabunge hapa gari ya uwanja wa ndege; ndege bado dakika kumi ndege itatua na moto unawaka, tunafanya nini? Lakini la kushangaza zaidi tunaambiwa gari moja ya zimamoto limetolewa Mbeya kupelekwa Dar es Salaam kwa matengenezo. Mimi huwa najiuliza gari hili hivi fundi hawezi kupelekwa Mbeya? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata kama lina mambo ya kiufundi, huyo fundi hawezi kwenda Mbeya akalicheki gari na baadae akarudi Dar es Salaam akachukua spea; gharama zake hapa zinakuwaje? Gharama za kupeleka gari Dar es Salaam na gharama ya kumpeleka fundi ipi ndogo? Lazima tukae wakati mwingine tuangalie haya mambo na pia tuyachukulie hatua zinazofaa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kulizungumza haraka ni huu msongamano unaozungumzwa wa magereza. Msongamano huu unasababishwa na mambo mengi likiwemo pia baadhi ya Wilaya zetu hapa nchini kukosa magereza kabisa. Niombe sasa tujitahidi hasa kule Chunya tupate magereza ili wafungwa sasa waweze kuwekwa kule na kupunguza msongamano kule Mbeya. Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba pia wenzetu wa Wizara ya Mambo ya Ndani katika kuyafanyia kazi mambo yenu haya muwape uwezo pia ndugu zetu wa polisi wa kule Chunya. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante ninaunga mkono hoja.