Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO A UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukushukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia hoja ya Kamati.
Kwanza, napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza sana Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji pamoja na Wajumbe wote wa Kamati kwa kazi nzuri ambayo wameifanya na hatimaye kutuletea ripoti ambayo imesheheni ushauri ambao ni mzuri. Kimsingi Kamati imekuwa karibu sana na sisi kama Wizara na tumeendelea kunufaika na ushauri wao, kwa kweli tunawashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge ambao kwa wingi wao wamechangia sana kuhusu masuala mbalimbali ya Wizara, masuala ya kilimo, mifugo na uvuvi. Inaendelea kuonesha namna gani Waheshimiwa Wabunge wanavyowajali wapiga kura wao ambao wengi wao ni wakulima, wafugaji na wavuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo machache, napenda kuchangia baadhi ya hoja za Waheshimiwa Wabunge, kwa vyovyote vile na kwa sababu ya muda sitaweza kumaliza yote. Ya kwanza kabisa ni kuhusiana na suala la migogoro ya ardhi kati ya wafugaji na wakulima na watumiaji wengine wa ardhi. Wizara inatambua fika kwamba hili ni tatizo kwa muda mrefu na imefika wakati kama wanavyoshauri Waheshimiwa Wabunge tatizo hili tukaondokana nalo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la migogoro ya ardhi ni suala mtambuka, linahusu Wizara zaidi ya moja. Ndiyo maana Serikali katika kuhakikisha kwamba tunalishughulikia tatizo hili imeunda Tume ambayo inashirikisha Wizara tano ikiwa inaratibiwa na Wizara ya Ardhi ili kwa pamoja tujaribu kuangalia migogoro hii ili hatimaye tuweze tukatafuta suluhu ya kudumu. Hivi tunavyozungumza, Tume hii ipo field na tayari imeshatembelea baadhi ya mikoa inawahoji wadau, inapitia ripoti mbalimbali za Kamati zingine za siku za nyuma kuangalia nini kilichosemwa na mwisho wake wataleta mapendekezo Serikalini ambapo na sisi tukishapata tutaleta mapendekezo kwa wadau mbalimbali mkiwepo ninyi Waheshimiwa Wabunge ili kwa pamoja tuangalie na tujadili namna gani ya kuweza kutokomeza hili tatizo ambalo kwa kweli limekuwa sugu kwa miaka mingi sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge muwe na subira, ripoti itakuja, inawezekana ikaonekana kwamba imechelewa lakini tatizo la migogoro siyo tatizo dogo limekuwepo kwa miaka mingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuzungumzia kuhusiana na hoja iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge kuhusu madeni na ubadhirifu kwenye Vyama vya Ushirika hususan kwenye vyama vya korosho. Wizara yangu inatambua kwamba ubadhirifu katika Vyama vya Ushirika inachangia sana katika kudidimiza kilimo na ndiyo maana tumekuwa tukichukua hatua mbalimbali kuhakikisha kwamba tunakabiliana na wote wale wanaofanya ubadhirifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni COASCO imekamilisha kupitia mahesabu ya vyama 200 Mtwara na Lindi na imebaini kwamba kuna upungufu mkubwa na kuna ubadhirifu mkubwa wa fedha za wananchi. Napenda kuwataarifu Waheshimiwa Wabunge wanaotoka Mikoa ya Lindi na Mtwara kwamba tupo njiani kwenda kuhakikisha kwamba tatizo hili linashughulikiwa na wale wote ambao wamehusika watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuvunja Bodi za Vyama vya Ushirika hivyo 200. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumzwa vilevile suala la Hifadhi ya Ngorongoro na Loliondo. Napenda kusema machache, Hifadhi ya Ngorongoro kama alivyosema Mheshimiwa Sakaya ni hifadhi ya kipekee sana duniani. Upekee huu pamoja na mambo mengine ni kwa sababu ni hifadhi ya pekee duniani ambayo binadamu anaishi kwa amani na wanyamapori. Hiyo ndiyo imeipatia Ngorongoro kuwa na sifa hiyo ya kipekee na Serikali inatambua hilo na inaendelea kushughulikia changamoto mbalimbali zilizopo ili tabia hii ya wananchi kukaa vizuri na wanyamapori iendelee kutokea.
Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.