Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN:Bismillah Rahman Rahim.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na kwa sababu ya dakika kumi ulizonipa basi niende haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ya kwanza ni kuhusiana na ufinyu wa bajeti. Kamati yetu sisi imeshindwa kutembelea maeneo ambayo hasa yana migogoro na kuweza kuishauri vizuri Serikali. Mgogoro wa Ngorongoro kila Mtanzania anaufahamu, Loliondo, lakini uvamizi katika mapori ya akiba ya Kigosi, Moyowosi, Burigi, Kimisi na kadhalika, kote huko tumeshindwa kufanya kazi kwa sababu ya ufinyu wa bajeti, Wizara yenyewe hadi hapa tunazungumza bado robo moja kumalizia ina chini ya asilimia 30 ya bajeti ambayo imetengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliombe Bunge hili, mtu anaonyeshwa njia wakati wa kwenda siyo wakati wa kurudi, bajeti ijayo tuhakikishe tunaweka fedha ya kutosha katika Kamati zetu na katika Wizara zetu ili tuweze kufanya kazi vizuri na kuishauri Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mweyekiti, suala la pili, tuna tatizo kubwa sana katika nchi yetu lakini tunalidharau na tukiendelea kulidharau kwa mujibu wa tafiti zinazofanywa na wataalam baada ya miaka 20 nchi hii tutalia kilio cha kusaga meno. Waheshimiwa misitu yetu inapotea kwa kasi kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana ndugu yangu Mheshimiwa Kiwanga alilia machozi kama mtoto mdogo alivyokuwa anatembea katika Kamati akaona misitu inavyoathirika. Labda nitoe mfano, uchomaji wa mkaa ni chanzo kikubwa sana cha nishati na asilimia 90 ya Watanzania wanategemea nishati ya mkaa na kuni kwa ajili ya matumizi yao ya nyumbani, lakini vitu hivyo havina sheria, kanuni na hakuna sera ya uchomaji wa mkaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano, kuna vijiji kumi Kilosa vimefanyiwa utafiti, wamepanga matumizi ya ardhi pamoja na matumizi ya misitu, wamegawa vile vijiji katika block 24 na kila mwaka wanatumia block moja kwa kuni, mkaa na matumizi yao. Kwa hiyo, miaka 23 wanaacha zile block zina-regenerate zenyewe. Kwa hiyo, pale tatizo lile limeondoka, faida yake nini? Hakuna uvamizi katika yale maeneo mengine, kijiji kinapata faida zaidi kutokana na mapato yanayopatikana, lakini pia kuna na ile teknolojia iliyowekwa pale ya uchomaji mkaa ile miti inatumiwa vizuri pamoja na majiko yale bunifu waliyonayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tusijidanganye, tujiulize, hivi ni miti mingapi inayokatwa kwa mwaka mmoja ndani ya nchi yetu na ni miti mingapi inayopandwa kwa mwaka ndani ya nchi yetu, inawiana? Huo mti utakaopandwa utakaa miaka mingapi ili tuje tukate tena? Kwa hiyo, tusijidanganye mtu anaweza akasema yeye hatumii mbao kwa sababu sasa hivi kuna teknolojia atatumia vioo kutengeneza milango, meza na kadhalika lakini akifa, nani ambaye haendi na ubao?
Kwa hiyo, tusijidanganye hii ni kwa wote Mkristo utaenda na sanduku, Muislam utawekewa ubao, kila mtu siku ya mwisho utaondoka na ubao. Kwa hiyo, miti ina faida kubwa ukiondoa zile tangible na intangible benefit kutoka kwenye miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu, hili ni janga, ni kubwa lakini bado Watanzania tunalifumbia macho. Hivi hatuumii kila siku kusikia ndugu zetu wanauana kwa sababu ya tatizo la wafugaji na wakulima?
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.