Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi nijikite katika masuala ya Jimboni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake najua wananisikiliza. Moja, kama ambavyo nilimsaidia Waziri wa Viwanda na Biashara babu yangu kwa wezi wale wa EPZ nawaambieni mkashughulike na wezi wa miradi ya maji, mmoja ni mtoto wa aliyekuwa kada wenu na Waziri mwenzenu wa zamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siyo kama wale wanaotajataja wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa zaidi ya shilingi milioni 800 Kata ya Kabasa, shilingi milioni 800 pesa za walipakodi, huyu mtoto, maji hakuna, kashughulikieni hilo tatizo. Nyamswa kwa Boni niliwaambia, ameharibu Mtwara ameharibu na maeneo mengine, huu mradi mkubwa ndiyo usiseme kabisa ilikuwa kila Serikali ikiweka hela wanakata benki moja kwa moja kwa huu utapeli. Rorya kule walimfukuza, wananchi wangu wa Bunda wanataka maji, nimeshasafisha Baba yao nasafisha na uchafu wote, sitaki nataka wananchi wa Bunda wapate maendeleo, hilo limeshaisha, nadhani mmeshanielewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunda kuna njaa, Baba wa Taifa alisema anayeficha maradhi kilio humuumbua, tuna njaa. Narudia, Bunda tuna njaa au niseme tu lugha laini, tuna upungufu wa chakula kwa kata zaidi ya sita. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, njaa hii siyo ya kujitakia, tatizo la tembo kuharibu mazao ya wananchi, dada yangu Mheshimiwa Jenista alishakuja kutembelea tukampeleka katika mashamba na moja ya shamba aliloenda kwenye Jimbo langu na akaahidi ataitisha kikao pamoja na Waziri wa Maliasili mpaka leo hicho kikao hatujafanya, dada yangu sijui kikao tutafanya lini, utanijibu uniambie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Bunda wamesema hawataki kuomba chakula, wana uwezo wa kulima msiwatengenezee njaa wasiyoihitaji. Tembo wenu wanatoka wanakula mazao kule sijui ndovu, sijui tembo, sijui mazagazaga gani mtajijua wenyewe, halafu tena tukiwaambia tuna njaa hamtaki tuseme tuna njaa. Naomba wananchi wangu biashara ya kuombaomba hawataki na ninyi mmesema Serikali yenu hamtaki kuombwa sisi hatutaki kuomba, mnatuchokoza wenyewe, tembo wenu wanakuja kula mazao yetu, marufuku. Nimeshasema hivyo na mtuelewe, tunaomba mlete chakula kwa sababu tembo wenu ndiyo wamesababisha matatizo yote haya. Hayo ndiyo yaliyonifanya nisimame nizungumze. Wananchi wangu wanataka chakula, kwa sababu kuna njaa iliyosababishwa na Serikali kwa tembo wao kuja kula katika mazao ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.