Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi kukushuru kwanza kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia Kamati ya Huduma ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, pamoja na Ardhi, Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kupongeza uchaguzi uliopita tarehe 22 Januari, 2017 ambapo Chama cha Mapinduzi kiliwafunga wapinzani wetu wana UKAWA goli 22 kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana unajua tunajuana humu ndani wapo wanaokula msuba asubuhi, mchana na jioni kwa hiyo hainipi shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niende kwenye suala la kilimo kwa maana ya ubora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba hiyo kazi wanayoifanya ndiyo iliyowaleta humu ndani na hawana kazi nyingine kama wangekuwa na kazi wangekuwa watulivu wasikilize nini kinachochangiwa sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ya Kilimo wawe makini sana kwenye suala la ubora wa mbegu. Mbegu zinazopelekwa kwa wakulima siyo mbegu sahihi, wakati mwingine mbegu zile huwa zinakuwa zina shida, hata kama ni mbegu ambazo zinatolewa kwa mtindo wa ruzuku lakini bado hazimsaidii mwananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukisema kwamba kunai le hali ya mimba za utotoni, kwenye mbegu hizi nyingine nazo ni staili ya mimba za utotoni. Kuhusu hizi mbegu unakuta wakati mwingine mbegu zinakuwa ni fupi haziwezi kuzalisha kadiri ambavyo inastahili, kwa hiyo Wizara ya Kilimo tunaomba muwe makini. Pia niseme endapo mbegu hizo zisizokuwa na ubora zinaletwa, mwisho wa siku mwananchi anapokuwa amepata hasara, hasara hii inafidiwa na nani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niongelee suala la mawakala wa pembejeo. Mawakala wa pembejeo hili ni jambo ambalo tumekuwa tukiliimba kila siku. Mawakala wa pembejeo ambao kimsingi waliikopesha Serikali, walifanya kazi ya kusambaza mbolea na mbegu mbalimbali kwa ajili ya kuikopesha Serikali mwisho wa siku mawakala hawa mpaka leo hawajalipwa. Toka mwaka 2014, mwaka 2015, mwaka 2016, ni lini Serikali hii itawalipa hawa mawakala? Wamekuwa na shida na wengine mpaka sasahivi wameshapoteza maisha na wengine wanadaiwa na mabenki, walikuwa wazima wakati wanakopesha mbolea hizi kwa wananchi, sasa hivi unakuta tayari wameshanunua magonjwa kama pressure. Naiomba Serikali iwe serious ili kuwasaidia hawa wananchi wajasiriamali ambao waliweza kuikopesha Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende pia kwenye Benki ya Kilimo. Wakati tunapitisha bajeti hapa mwaka jana mwezi wa sita, bajeti ya kilimo, Waziri alikuwa amesema kwamba angeweza kufikisha Benki ya Kilimo katika Mkoa wetu wa Ruvuma, lakini nashangaa mpaka sasa hivi bado haijafika, sijui ndiyo bado upembuzi yakinifu au ni nini? Mpaka sasa hivi hakuna dalili zozote zile za kufikisha benki hii ya kilimo! Niombe Waziri wa Kilimo tafadhali kwa kuwa mkoa wa Ruvuma ni mkoa ambao wananchi wake wanashugulika na kilimo kwa asilimia 92, naomba sasa benki hii iende ili iweze kuwasaidia wananchi hawa waweze kukopa na kuweza kufanya uzalishaji wenye tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la uvuvi; tunalo Ziwa Nyasa katika Mkoa wetu wa Ruvuma. Mimi naomba nishauri jambo hapa, uvuvi katika Ziwa Nyasa samaki walioko pale wangeweza kuwa wengi zaidi na uvuvi ule ukawa na tija endapo kama Serikali ingeweza kufanya kama wanavyofanya wenzetu wa Malawi, kwa sababu ziwa hilo moja liko upande Malawi na upande mwingine wa ziwa upo upande wa Wilaya ya Nyasa kwa maana ya Tanzania. Kwa hiyo, wenzetu wa Malawi wanachokifanya wanalisha chakula kwenye lile ziwa, samaki wanakwenda kwenye upande wa Malawi kwa sababu kuna chakula. Wenzetu wa Malawi sasa wanapata mavuno mengi kutokana na hili Ziwa Nyasa. Sisi tunaambulia patupu, ziwa lipo tunaambulia kuangalia tu mandhari ya ziwa lilivyo lakini hatuna faida nalo yoyote ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali ione umuhimu kama tuko serious na suala hili la uvuvi, basi walao tufanye huo utaratibu wa kuwa tunalisha chakula ili tuweze kupata samaki wazuri ambao tutawauza na watatupatia pato…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante Jacqueline.