Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba ku-declare kwamba mimi ni mdau wa utalii na nitaanza na suala zima la hali ya utalii nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyotambua, utalii ni kati ya sekta ambayo inachangia katika pato la Taifa kwa asilimia 17.5, lakini nasikitika na naona kwamba asilimia hizi zitapungua. Mheshimiwa Waziri wakati akijibu hoja tulivyokuwa tunachangia Kamati ya Bajeti alisema ongezeko la VAT halikuathiri wageni kuja nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mdau; wageni wengi waliokuja mwaka jana; VAT tuliipitisha hapa Bungeni mwezi wa Sita na Sheria ikaanza kutumika mwezi wa Saba; watalii wanatoka nchi mbalimbali wengi walikuwa wameshaanza kusafiri kuja nchini Tanzania, kwa hiyo walikuwa wamesha-book package zao. Kwa vyovyote vile mgeni anakuja mpaka hapa Tanzania amefika unamwambia kwenye package yako na kuongezea eighteen percent hawakubali. Sasa badala yake wale local tour operators ndio waliolipia zile fedha za zaidi na badala ya kuwasaidia Watanzania mmezidi kuwaumiza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningependa ili tuweze kupata figure halisia baada ya mwaka huu tujue ni watalii wangapi wamekuja. Kwa mfano compare Januari mwaka jana na Januari mwaka huu tuone ni watalii wangapi wamefika. Mimi nipo kwenye sekta hii na Januari mwaka huu sasa hivi mahoteli ni matupu hakuna wageni, tujiulize ni kwa nini hakuna wageni? Kule kilimanjaro huwa tuna-run Kilimanjaro marathon; Kilimanjaro marathon ni international inaleta wageni wengi sana hapa Tanzania. Baada ya kukimbia huwa wanapanda mlima, wanaenda safari na wanaenda kwenye beach tours; lakini mwaka huu wageni ni wachache, mahoteli bado hayajajaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba muangalie ni kwa nini wageni hawa hawaji tena Tanzania wanaenda nchi jirani, wanaenda Mombasa. Tuna wanafunzi huwa wanakuja Tanzania kama volunteers wale wanafunzi they are about sixteen to eighteen years old, wanakuja, wazazi wao wanajitolea, wanakuja kwa three weeks holiday; wazazi wanajitolea, wanachangisha fedha wanakuja wanasaidia kwenye kujenga mashule kupaka rangi na kadhalika, lakini hapa Tanzania tumekuwa tukiwachaji work permit ya dola mia tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke wale wanafunzi wakija wanalipa visa fee ya Dola hamsini, bado wakikaa hapa kwa wiki mbili wanapanda mlima, wanaenda safari na wanaenda mpaka Zanzibar. Sasa wazazi wao wamejitolea kuja kutusaidia Watanzania lakini wanachajiwa dola mia tano kwa kuja kujitolea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali mliangalie hili kwa sababu tunapoteza wageni wetu. Mwaka huu nilikuwa na wageni zaidi ya mia saba lakini wote wame-cancel wanaenda Mombasa, tutapata wageni karibu hamsini tu. Naomba Serikali iliangalie hili tujaribu kuondoa ile permit visa ya dola 500 atleast mchaji reasonable price, labda hata kama dola mia moja hivi itakuwa ni fair, lakini dola mia tano ni nyingi sana tukumbuke na wale ni wanafunzi na wale wazazi wanakuja kutusaidia sisi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tunaamini michezo ni afya na kama Bunge la Tanzania ningefurahi sana tarehe 26 mwezi wa Pili kuwaalika Wabunge na nyie mje mkashiriki kwenye Kili Marathoni; mnaweza mkakimbia zile kilomita tano kama sapoti kwa sababu zile ni fun run mnaweza mkatembea ama mkakimbia, lakini itakuwa na sisi kama Watanzania tumeonesha moyo katika haya mashindano ya Kimataifa ambayo watu wanatoka all over the world lakini sisi kama Watanzania na kama Bunge la Tanzania bado wengi wetu hatujaweza kwenda katika mashindano yale.