Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nishukuru kwa kunipatia nafasi
ya kuweza kuchangia katika Wizara hizi mbili. Nizipongeze Wizara zote hizi mbili na Kamati kwa
kazi kubwa zilizofanyika kwa ujumla wake na tunaweza kuchangia hapa kwa sababu kuna kazi
ambayo imefanyika na tunaiona.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la REA. Suala la REA kazi kubwa imefanyika,
lakini bado tunaomba Wizara ifuatilie kwa karibu. Nasema ifuatilie kwa karibu kwa sababu REA II
ambako umepita, umeme umepita barabarani tu. Nguzo zimeingia kidogo sana na jambo hili
tumekuwa tukilizungumza kwa nyakati zote. Kwa hiyo, hao wakandarasi wanapofanya kazi
inabidi wafuatiliwe. Ukienda sehemu kama za Kinyangiri na Ngalakala, maeneo yote yale
umeme haujaingia sana ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine katika Wizara hiyo nizungumzie suala la
madini. Sisi kule Mkalama tumepata madini ya gypsum na madini mengine ya shaba yapo,
lakini kinachotokea ni kwamba watu wanakuja na leseni wanaanza kuchimba madini bila kuwa
na utaratibu. Tunaposema utaratibu, maana yake waje, waonane na vijiji husika, wakionana na
vijiji husika basi kunakuwa na utaratibu wa kuanza kufanya kazi hiyo bila manung‟uniko. Sasa
hao watu wanaopata leseni wanakuja huku wanatuletea migogoro na Maafisa Madini wa
Mkoa wao wanawapa barua tu wale watu wanakuja lakini lazima uweke utaratibu mzuri
kurekebisha jambo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nikienda kwenye suala zima la barabara, kwanza
kwenye ukurasa wa 53 wamesema kuna barabara mikoa ambayo haijaunganishwa kwa lami
lakini sikusikia Simiyu wala Singida. Nafikiri ilikuwa ni mfano tu sasa tusiwe tunasahaulika Simiyu na
Singida, ni jambo la muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine; suala la alama za barabarani. Sasa hivi
kumekuwa na mgogoro mkubwa, alama nyingi zimepelekwa chuma chakavu. Mimi nafikiri
kama Kamati ilivyopendekeza sheria itungwe, lakini pia hatua zichukuliwe, kuwa na nguzo za
saruji labda inaweza ikasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spik ukienda Mlima Saranda pale kila siku wanafanya ukarabati
kwenye Mlima Saranda, zile kingo zinagongwa kila siku, ukarabati huo una gharama kubwa.
Sasa hakuna njia mbadala au kuna tatizo gani pale? Ziwekwe kamera tuone labda watu
wanakuja kwa mwendokasi ndiyo maana ajali zinakuwa nyingi, ukarabati wa zile kingo naamini
kabisa unagharimu pesa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya barabara inayogharimiwa na Serikali yakiwemo
madaraja, pia likiwemo Daraja la Sibiti. Miradi hiyo imekuwa inachelewa kwasababu pesa za
ndani haziji kwa wakati na jambo hilo limezungumzwa na Kamati. Serikali inabidi ione athari
zake, kwamba gharama za mradi zinaongezeka ikiwepo gharama wakandarasi na wale
washauri waelekezi, limekuwa ni jambo kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia wale wataalam washauri wamekuwa na tabia ya
kuegemea upande wa mkandarasi Kamati zikienda. Kwa nini hawawi upande wa Serikali ili
kuweza kuona ubora wa miradi? Jambo hilo ni muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine la barabara TANROADS, watu wanajenga
kwenye maeneo...
(Hapa kengele ilia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, naunga mkono hoja.