Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru kwa kunipa nafasi.
Kwanza nianze kwa kutoa pole kwa Wana-CCM wenzetu ambao walipata ajali na kupoteza
maisha kule Mkoa wa Kilimanjaro. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aweke roho zao mahali
pema peponi na pia awape moyo wa subira familia zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo napenda niende haraka haraka
katika kuchangia hoja. Suala la kwanza nilitaka kumuuliza Waziri wa Miundombinu, hivi zile
Bombadier Mtwara zitaenda lini? Mimi nimezipanda kwenda Tabora, nimepanda kuja Dodoma,
kwa kweli ni ndege nzuri zinaenda kwa kasi, zinachukua muda mfupi sana. Mtwara ni miongoni
mwa viwanja bora sana ambavyo vimejengwa muda mrefu, kwa nini na sisi tunyimwe hiyo haki
ya kupelekewa Bombadier? Kwa hiyo, nilikuwa naomba atueleze lini hizo Bombadier zitaanza
kwenda Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo lingine nililotaka kulizungumzia ni kuhusu barabara ya
kutoka Mbwenkulu kwenda Nangurukuru. Kwa kweli ile barabara kile kipande kimechakaa,
kinatitia na kinasababisha ajali nyingi sana. Ukitoka Somanga kwenda Daraja la Mkapa kile
kipande ambacho kimejengwa na Caraf unaweza mpaka kuandika hata barua, yaani huwezi
kujua kama uko kwenye gari. Tunaomba na eneo lile la kutoka Mbwenkulu kwenda
Nangurukuru nalo lirejewe na liwe na ubora ule ule unaofanana kutoka Somanga kwenda
Darajani. Huwezi kuamini kama uko ndani ya gari. Tunaomba kwa kweli lile eneo lirudiwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine ambalo nilitaka nilizungumzie ni kuhusu umeme.
Katika Mji wa Mtwara juzi nimepokea message kwamba wanaomba samahani kwamba siku hizi
kuanzia saa moja mpaka saa nne usiku hakuna umeme. Sasa hivi anaeanza kupata umeme
kuanzia saa tano huo kweli si afadhali hata tungekuwa tunapewa saa moja mpaka saa nne?
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachosababisha ni kwamba zile megawati 18 zimeshakwisha
sasa hivi, kwa hiyo ikitokea shoti kidogo kwenye jenereta moja ni tatizo. Tunaomba yaongezwe
majenereta hali ni mbaya katika Miji ya Mtwara na Lindi. Tunaomba Wizara ya Nisahati ije na
kauli inaongeza lini megawati lakini hata ile mitambo iliyopo wanaifanyia lini matengenezo ya
uhakiki? Huwezi kuwa na mahitaji megawati 18 na zilizopo megawati 18. Kwa kweli hapana,
tunaomba hilo waliangalie. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na suala lingine ambalo nilitaka nilizungumzie ni suala la
barabara kutoka Mtwara kwenda Newala - Masasi ni kilometa 30, tunataka kujua mkataba
unasainiwa lini Mheshimiwa Waziri? Mheshimiwa Rais alituambia akiingia madarakani kazi ya
kutoka Mtwara Mnivate inaanza na eneo lililobaki ataweka wakandarasi wanne ili wajenge kwa
wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba vile viatu vya Mheshimiwa Rais, ambaye alikuwa
Waziri wa Ujenzi aliyekutangulia ujitahidi ili viweze kukuenea.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.