Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Kwanza naomba
kupongeza Kamati zote mbili kwa taarifa zao nzuri, lakini naomba nianze na tatizo la umeme
kwenye Mji wa Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kila siku umeme Geita unakatika kila siku zaidi ya mara nne.
Nimezungumza mara nyingi sana na Waziri, nimezungumza na Naibu Waziri na tatizo hili kwa
zaidi ya miezi nane halipatiwi majibu. Nafahamu kuna mradi ambao unaendelea lakini nadhani
speed ya mradi huo ni ndogo sana, kwa hiyo, nilikuwa naomba sana Waheshimiwa Mawaziri
wanisikie kwamba kuna tatizo kubwa sana la umeme katika Mji wa Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili, mji wenyewe wa Geita ule, ni nusu peke yake ndiyo
unaowaka umeme, sehemu zingine umeme hakuna. Tunaambiwa tunasubiri umeme wa REA na
niliongea na Naibu Waziri nikamuomba basi atupe ratiba ya mradi wa REA wa nchi nzima tujue
kwamba Geita unakuja lini.
Mheshimiwa Naibu Spika, linguine pamekuwepo na malalamiko mengi sana kwamba
watu wanalalamika kwanini Geita uwanja wa ndege umejengwa Chato? Sisi watu wa Geita
ndiyo tunajua. Mheshimiwa Rais akitokea Geita kwenda Chato ni kilometa 160. Ili afike Chato,
magari yanayotangulia mbele yanasimamisha watu matokeo yake kwa saa sita watu
wamesimama Barabarani. Kwa hiyo, solution ni kumjengea uwanja karibu na nyumbani
kuondoa ule usumbufu. Kutoka Geita kwanda Chato ni kilometa 160 kwa hiyo, watu
wanaolalamika kujengwa uwanja Chato ni kwa sababu hawafahamu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hili, nilikuwa naiomba tu Wizara ya Mawasiliano isiondoe
sasa nafasi ya kutujengea uwanja wa Mkoa wa Geita kwa sababu hatuwezi kuzuia Mheshimiwa
Rais ule uwanja usijengwe kule. Hata usipojengwa kero yake ni kubwa sana kwa wananchi pale
barabarani.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la tatu, Mheshimiwa Rais Mgodi ule wa Geita karibu
miaka kumi ijayo utakuwa umeshachimba dhahabu. Geita hii tunayoizungumza ambayo kwa
Mgodi ule ndiyo the leading gold producer hapa Tanzania na karibu ya pili Afrika, wananchi
bado ni maskini. Na ukitazama, sioni dalili za namna ambavyo huu mgodi utabadilisha maisha
ya Wananchi sasa hivi kwa muda mfupi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kwa Serikali, wangeanzisha mfuko wa natural
resources rent extraction ambao unafanyika katika nchi nyingi sana. Kwa mfano, mfuko kama
huu upo Norway, mfuko kama huu upo Marekani. Wakati kazi za madini zinapokuwa
zinaendelea, mfuko maalum kwa ajili ya kuwafanya wananchi wa maeneo yale baada ya
shughuli za madini kuisha waweze kuendelea na mambo mengine unakuwa umeandaliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunavyokwenda sasa hivi, kesho kutwa dhahabu zitakwisha
kama zinavyoisha Kahama, wananchi watabaki maskini, Geita hatuna hospitali, Geita hatuna
barabara, Geita hatuna maji, Geita hatuna kila kitu lakini dhahabu zipo nyingi. Kwa hiyo,
nilikuwa nafikiri kwamba kuna tatizo hapa, siyo suala la kwanza duniani ni tatizo ambalo watu
wengi wameshindwa kulisemea hili. Tukianzisha mfuko huu ambao utatusaidia watu wataweza
kusoma, utaweza ku-deal na humanitarian crisis lakini utaweza kushughulika pia na mambo
mengine ya development kwenye maeneo yale. Sasa hivi tunapata 0.7 CSR kwa miaka 17,
mgodi umejenga shule moja ya wasichana. Kila siku wanaonesha kwenye television, miaka 17
0.8 percent ya CSR wangeweza kuifanya Geita kuwa Ulaya, lakini kwa sababu wanaamua
wenyewe wafanye nini hakuna kinachooneka kimefanyika pale. Maisha ya wananchi wa Geita
inaendelea kuonekana kama vile hawapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya muda nashukuru kwa kunipa nafasi.