Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipatia fursa hii ili niweze kuchangia lakini zaidi nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuchangia hoja hii. Naunga mkono taarifa ya Kamati na ushauri uliotolewa na Kamati ni mzuri sana na moja; wameshauri juu ya umuhimu wa kulipa deni. Ni hoja na ushauri mzuri sana kwa sababu usipolipa deni madhara yake ni makubwa sana mbali ya haya yanayoweza kujitokeza kwa hawa ambao wameikopesha Serikali, lakini pia gharama zinaongezeka pale ambapo wanaotudai wanaweza wakatupeleka hata Mahakamani, kwa hiyo gharama zinaongezeka kwa hiyo ushauri ule ni mzuri, sisi tunaupokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nililotaka kuchangia ni suala tu la namna ambavyo Waheshimiwa Wabunge tunajenga hoja hapa. Kanuni zinatukataza wakati wa mijadala kutumia jina la Rais kwa dhihaka katika mijadala au kwa madhumuni ya kushawishi kufikiwa maamuzi fulani. Kwa hiyo, naomba tu nikumbushe Wabunge wanapokuwa wanashiriki kutekeleza jukumu lao la Kikatiba la kuishauri na kuisimamia Serikali wanapojenga hoja, wajenge hoja kwa namna ambavyo pia haikiuki kanuni tulizojiwekea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tu kusema kwamba kauli za Rais na Viongozi wengine tuzitazame katika muktadha wa yale anayozungumza katika contextual meaning kuliko una-peak tu sehemu fulani halafu unalipotosha kabisa lile kusudi lililokusudiwa. Kwa hiyo, nishauri hivi; tunatambua Katiba imeweka uhuru, haki ya kila mtu kuwa na uhuru wa mawazo na fikra zake, ni jambo la msingi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na haki hiyo lakini tuitumie vizuri kwa kuangalia muktadha wenyewe wa ile kauli yenyewe, tusipotoshe. Kwa mfano, Mheshimiwa Lwakatare amezumgumza aliyozungumza Rais kuhusu ngono au katerero, amekiri kabisa kwamba yale mambo yapo Bukoba na watu wanaweza kwenda kujifunza kule na kiko Kijiji mahususi kwa ajili hiyo, lakini ukweli ni kwamba Rais alikuwa anazungumzia ngono na katerero? Hapana.
Kwa hiyo, ushauri wangu ni kwamba Waheshimiwa Wabunge tunapotumia haki yetu ya Kikatiba ya kuwa na uhuru wa mawazo na fikra, basi tutoe tafsiri sahihi kwa kauli zinazotolewa na viongozi wa Serikali kwa kuzingatia muktadha wa kauli hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana.