Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naomba nichangie. Kwanza nawashukuru sana na nawapongeza sana Kamati kwa kazi nzuri ambayo wamefanya kwa sababu, kwa kweli, wamezungumza kitu kile ambacho kinapaswa kuzungumzwa.
Mheshimwa Mwenyekiti, watu wengi wameshazungumza kuhusiana na deni la Taifa. Naomba niweke mstari tu kwamba sisi kama Bunge tusiposimama kwenye nafasi yetu na kuiambia Serikali kinachopaswa kufanyika, tunaweza tukajikuta tuko kwenye hatari kubwa na tukawa mufilisi; tukawa hatuwezi kukopesheka na tukawa vile vile hatuwezi kuhudumia Watanzania ambao tunapaswa kuwahudumia. Hii ni kwa sababu ukiangalia kwenye maandiko ya Kamati inaonesha kwamba deni linakua kwa asilimia 18. Hili ni jambo la hatari.
Mheshimwa Mwenyekiti, wakati deni hili linakua, kuna mambo ambayo yanafanywa na Serikali ambayo yangeweza kufanywa kwa namna nyingine ambayo ingeweza ikawa na tija zaidi kwa Serikali. Kwa mfano, tumenunua ndege kwa pesa taslimu; ule ni mradi wa kibiashara ambao ungeweza ukaachwa ukakopa wenyewe, ukajiendesha wenyewe, uka-service hiyo riba wenyewe; lakini tumeenda kununua cash.
Mheshimwa Mwenyekiti, lakini wakati huo huo tunakopa, tena tunakopa ndani kwa kiwango ambacho ni kinyume hata na kiwango kilichoidhinishwa na Bunge hili. Maana yake ukiangalia huku, tumekopa tukazidisha asilimia 32. Naomba sana Bunge hili lisimame mahali pake liiambie Serikali iache tabia za aina hiyo, kwa sababu inakwenda kutuingiza kwenye hatari ambayo itakuja kuwa tatizo kubwa sana. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, kutokupeleka fedha kwa wakati kwa miradi mbalimbali, hili ni jambo lingine ambalo linaonekana kama ni rahisi tu; lakini ukweli ni kwamba usipopeleka fedha kwenye mradi kwa kadri ilivyoelekezwa, maana yake unalipa watumishi wengi bila kazi yoyote. Unakuta watu wapo kwenye Serikali, mashirika mbalimbali na Halmashauri, hawana kazi ya kufanya, lakini mwisho wa mwezi lazima walipwe mishahara. Sasa tukiendelea na tabia hii, tunakwenda kwenye jambo ambalo ni tatizo kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwenye kuchelewa kupeleka fedha au kushindwa kupeleka fedha maana yake ni nini? Miradi ile ambayo ilikusudiwa, gharama zake za kuitekeleza zinaongezeka na mahali pengine inaleta migogoro. Unakuta mahali ambapo kulipaswa kufanyiwe fidia ya labda shilingi bilioni 10, unaambiwa sasa ni shilingi bilioni 20 na hiyo gharama kwa vyovyote inabebwa na Serikali na kodi za wananchi. Kwa hiyo, tunaendelea kuweka mzigo mkubwa zaidi kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa nilizungumzie, ni kuwa na mipango mingi ambayo kimsingi haitekelezeki. Kwa mfano huku, unaona mahali ambapo Kamati imebainisha kwamba miradi ambayo inapaswa kutekelezeka; kwa mfano, mradi wa makaa ya mawe Mchuchuma na Liganga, hili ni jambo ambalo lipo kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwamba jambo hili pamoja na kwamba wamesema linaweza likatekelezwa robo ya kwanza ya mwaka huu wa fedha. Jambo hili halitawezekana kwa sababu mpaka sasa hivi fidia peke yake ya kuwahamisha wale wananchi ambao wanapaswa wapishe mradi huu haijafanyika. Kama haijafanyika, ukiangalia urasimu unaotakiwa kwa vyovyote haitawezekana kukamilisha hilo zoezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba tunakuwa na vitu vingi ambavyo hatuwezi kuvitekeleza. Tunashindwa kuwa na vipaumbele. Kwa hiyo, nashauri kwamba tuwe na vipaumbele vichache ambavyo tuna uwezo navyo na hivyo vipaumbele, kwa sababu Serikali ilishasema kwamba mradi huu ni wa kimkakati, maana yake ingekuwa ni jambo la busara sana kama Serikali ingeelekeza nguvu zake zote kwenye haya mambo machache ambayo yana input kubwa kwenye uchumi wetu ili yakifanyika, tuweze kupiga hatua haraka na tukaendelea kweli kama ambavyo inaelezwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiendelea na hadithi hizi za kwenye makaratasi za kueleza kwamba hili litafanyika halafu, yaani kama bluffing tu, kwamba “funika kombe mwanaharamu apite,” yaani tunaliambia Bunge kwamba jambo hili litatekelezeka, lakini ukweli ni kwamba inaendelea kuwa hadithi. Nimemsikia Mheshimiwa Ndassa akisema, kwa sababu Mheshimiwa Ndassa ni mtu senior sana kwenye hili Bunge, kwa maana ya kukaa muda mrefu kwenye hili Bunge; akisema hiyo hadithi, kwamba toka ameingia Bungeni na labda ataondoka Bungeni, huo wimbo umekuwepo wa Mchuchuma na Liganga. (Makofi)
Mheshimwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba sana sasa tupige hatua, tuwe na vipaumbele vichache ambavyo tunaweza kuvifanyia kazi, bajeti ambayo ni realistic, inayotekelezeka na tuifanye kulingana na time. Kitu kingine ambacho kinasikitisha sana ni kwamba mambo haya yanashindikana, lakini yapo mambo ambayo hayajapangiwa bajeti; hayapo mahali popote, unaona yanatekelezwa.
Mheshimwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Rais akiwa kule Magomeni anasema natoa shilingi bilioni 10 kujenga nyumba; lakini huu mradi wa Mchuchuma kwa ajili ya fidia inayotakiwa pale ni shilingi bilioni 15. Hivi ni kwa nini hakushauriwa kwamba hili jambo la kwenda kufanya fidia kule mchuchuma ni la muhimu zaidi kuliko kwenda kujenga nyumba pale Magomeni? Kwa hiyo, naomba sana Bunge lako liibane Serikali katika jambo hili ili haya mambo yaweze kufanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la uzito unaotakiwa kutolewa kwa ajili ya sekta binafsi. Sekta binafsi ina mchango mkubwa sana kwa uchumi wetu. Nafikiri zaidi ya asilimia 57 ya uchumi wetu unategemea sekta binafsi. Ukiangalia mwenendo wa Serikali ya Awamu ya Tano kwenye suala la sekta binafsi, ni kana kwamba tunarudi kwenye ujamaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia juzi hapa kwamba, limetolewa agizo kuwa nyumba zote za Serikali sasa hivi zitajengwa na Tanzania Building Agency. Hii ni kampuni kama kampuni nyingine; na kimsingi agency hii kazi yake siyo kujenga.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni lazima tuishauri Serikali na Serikali iwe wazi, ituambie tunakwenda wapi? Sisi tunakwenda kwenye ujamaa au tunakwenda kwenye ubepari au tunakwenda kwenye ile mixed economy. Kwa sababu kimsingi ni kama tumechanganyikiwa hatujui tunapokwenda. Sasa matokeo yake ni kwamba tunaua private sector.
Mheshimwa Mwenyekiti, dada yangu hapa, Mheshimiwa Esther Matiko amezungumza habari ya madeni ambayo yanaibana sekta binafsi. Hili la kuibagua sekta binafsi kwenye kandarasi za Serikali na lenyewe linaua private sector ambalo ni tatizo kubwa na inaweza ikatuletea matatizo makubwa kwenye uchumi wetu.
Mheshimwa Mwenyekiti, hatupaswi kushangaa ni kwa nini uchumi unadorora…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.