Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

kunipa na mimi nafasi ya kuchangia kwenye taarifa ya Kamati. Awali ya yote niungane na walioipongeza Kamati kwa kazi nzuri walioifanya ya uchambuzi na kutupatia mwelekeo, huenda bajeti ijayo ikawa nzuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati imefanya kazi kubwa ya kutuonesha maeneo gani tunapaswa kuyafanyia kazi kama nchi, Kamati imetusaidia kutuonesha hali halisi ya nchi yetu iko wapi katika masuala ya kiuchumi na vilevile kutuwekea mazingira mazuri ya kutuwezesha kufanya tathmini na kujipanga kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuipitia taarifa hii nimeona kuna mambo mawili, matatu tunapaswa kujifunza na wataalam wetu watusaidie. Sina hakika kama tumewahi kujiuliza swali kitu gani kinacho-run uchumi wa nchi yetu. Ukiangalia kwa umakini vipimo vinavyotumika kuielezea Tanzania inaendelea au haiendelei ukitafakari kwa makini unakuja kugundua tunaishi Kitanzania na tunafikiri Kiulaya. Mwisho wa siku tukitafsiri fikra za Ulaya kwenye maisha ya Kitanzania tunakuja na majibu kwamba uchumi unakua halafu tunaona idadi ya maskini inaongezeka. Kwa nini hili linatokea? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya World Bank inaeleza itakapofikia mwezi August inflation rate itashuka, inaweza ikafika 4.5 kutoka kwenye 6.5. Hata hivyo, katika kipindi hiki uchumi wa nchi yetu unaonekana unaendelea kuimarika na wakatoa sababu kwa nini tunaendelea kuimarika. La kwanza wanalolisema ni kwamba Tanzania ina political stability nzuri yaani nchi yetu ina utulivu wa kisiasa kiasi kwamba tuna fursa zote za kufanya nchi yetu ikaendelea. La pili, nchi yetu ina fursa za kiuchumi nyingi za kutosha ambazo bado nyingine hazijatumiwa katika kiwango cha kusema hii nchi ni kuzimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unaposema kiwango cha umaskini kimeshuka halafu taarifa hiyohiyo inakwambia maskini wanaongezeka unaweza ukasema hii hai-make sense, ni kwamba tumeshindwa kutafsiri maisha ya Watanzania. Hivi kuna utafiti gani umefanyika baada ya kujengwa kwa barabara ya Dodoma - Iringa kupitia Mtera ukafika katika vile vijiji vilivyojengwa baada ya ile barabara wanauza nyama za mbuzi pale, kuna mtu ameweza kujua pato lao kwa siku ni shilingi ngapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu amewahi kufika Mbinga akakuta matuta kumi ya viazi yanayomfanya mwananchi pale aishi akienda dukani anakwenda kununua tu sabuni, chumvi na mafuta ya taa, akakaa Januari mpaka Desemba akauza magunia yake mawili ya mahindi akampeleka mtoto wake shuleni akasoma halafu mwisho wa mwaka mnasema huyu kwa siku yuko chini ya dola, vipimo gani tunavyovitumia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba wataalam wetu mtusaidie. Katika kipindi hiki nchi yetu imeendelea sana ndiyo maana wanasema uchumi wa nchi unakua. Anayesema maisha ya Watanzania hayakui ni kwamba hajakwenda into details, hajaenda kuangalia familia kwa familia tukoje. Hivi tuseme ule ukweli, kama kweli hapa ndani wote tuna familia na kuna watu tunawalea, kama tupo chini ya dola kweli tungeishi? Mnaelewa maana ya chini ya dola, maana yake tunaishi chini ya Sh. 2,000 kwa siku mtu ana familia ya watoto saba hakuna mtu anayekufa na njaa, does it make sense? Kuna vitu vingine mimi sivielewi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe wataalam, tukitaka tulingane na nchi nyingine zilizoendelea kama Asian Tigers, tukiwafuata tutapotea. Tukitaka tukajifunze Botswana kama wengine wanavyosema tutapotea. Mfumo wa Tanzania ni wa kipekee, unahitaji study yake ya kipekee utaleta matokeo tunayoyataka. Tukienda hivi, wachumi hawa wamesoma sana wamekuja na makabrasha na hawa si ndiyo walioshauri bajeti iliyopita, si ndiyo hawa wanaokuja na vyanzo vya mapato vilevile!
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niseme kabisa, tunahitaji a serious discussion, we need serious research kuhusu uchumi wa kipekee wa Kitanzania unapoishi na watu wanaoishi chini ya dola wakati huohuo wakaweza kusomesha, wakaweza kula, wakaweza kujenga, hii hali sio ya kawaida. Tutadanganyana tu na haya makaratasi hapa, tunasema uchumi umepanda, uchumi umeshuka, tutapelekwa kulia, tutapelekwa kushoto hatutafika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nikasema, kinachotutesa sisi na narudia tena, ni kufikiri Kitanzania, kuishi Kitanzania lakini tunadhani kwamba mifumo ile ya Ulaya ya uchumi ndiyo inayofaa kutafsiri uchumi wetu. Mipango ya Ulaya ya kukuza uchumi na projection zao ndiyo tunadhani zinatufaa kwa Watanzania, zimefeli na hazikuwahi kufanikiwa kutuletea majibu yanayotakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nenda kaangalie hali ya maisha ya kawaida ya Mtanzania, sawa, kuna vitu kama nchi lazima tuvifanye, tukivifanya hivyo tuna uhakika ile gap inayoonekana watu kuongezeka kuwa maskini kwenye maandishi ikapotea ni kwenye suala la infrastructure. Bajeti zijazo zijielekeze kwenye infrastructure, reli ya kati iimarike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi reli ya kati ilipokuwa inafanya kazi mtu wa maisha ya chini alikuwa anakula wale dagaa wanaotoka Kigoma, walikuwa wakifika Dar es Salaam ndiyo chakula kinachokuwezesha kuishi, unanunua kilo moja kwa Sh. 200, 300 leo hii kilo moja ya dagaa wa Kigoma anayeweza kula ni from royal family, kwa nini? Kwa sababu reli ya kati imeshindwa kuleta ule mtiririko uliokuwa una-cover matatizo mengine. Sasa tukiimarisha reli ya kati haya mambo mengine yote yatakwenda vizuri. Tukifungua barabara, kama nilivyosema, leo mimi nikitoka Dar es Salaam kwenda Mbinga sihitaji kupita Iringa, nitapita Masasi nitaongea na Ndugu yangu Mheshimiwa Mwambe dakika mbili nasonga mbele naingia Mbinga haraka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hali kama hii, leo inapasuliwa barabara hii ya Arusha kwa kupitia Msalato unapunguza kilometa nyingi ambazo tulikuwa tunazitumia kwenda Singida. Hali kadhalika ukatoboa barabara ya Kigoma – Mpanda – Sumbawanga na ukatoka Sikonge – Mpanda ukaja Tabora utaratibu unakuwa mzuri. Haya ndiyo maendeleo, tusiende kwenye hizi figures ambazo zinaonesha namba, hazina uhalisia katika hali ya kawaida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nakubali maendeleo ni watu, hatuwezi kusema kuna maendeleo ya vitu tukayatofautisha na maendeleo ya watu. Tukawa na barabara, viwanda, watu wakawa wanasononeka hawana furaha wanaishi maisha ya hovyo, haya siyo maendeleo. Maendeleo ya nchi yetu ni maendeleo ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante