Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi pia naomba niungane kuchangia kwenye hii kamati ya Bajeti. Kwanza nililokuwa nataka nichangie baada ya kupitia hii taarifa nimeona tumejikita sana kuzungumzia robo ya kwanza ya bajeti ya mwaka 2016/2017, lakini sote tunatambua kwamba pesa za maendeleo zimechelewa sana huko vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, ninaangalia kwenye bajeti yetu ya mwaka 2016/2017 tulipanga shilingi bilioni tisa kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri yetu ya Uvinza, lakini hadi sasa tunavyoongea mwaka jana mwezi Disemba tumepokea shilingi bilioni mbili, sawa na asilimia 22. Sasa ninajiuliza maswali, hivi kweli tutatekeleza vipi hii miradi ya maendeleo maana sasa tumeinga mwaka wa pili tangu tuchaguliwe huko na tuliahidi mambo mengi. Kwa hiyo, ninaomba kwenye Kamati hii ya Bajeti nimeona imeshauri sana, lakini haijafikia makubaliano na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nilikuwa naangalia ukurasa wa 10. Ukiangalia ukurasa wa 10, Fungu Namba 49, Wizara ya Maji na Umwagiliaji unaona kabisa kwamba kulikuwa na hoja ya kuongeza tozo kwa kila lita ya mafuta, petroli na dizeli, kuongeza 50 ili ifike 100. Lakini lengo la Kamati ilikuwa ni kwamba fedha hizi zipelekwe kwenye Mfuko wa Miradi ya Maendeleo ya Maji Vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia matokeo ya ushauriano Kamati inasema haijafikia makubaliano na Serikali. Sasa naanza kujiuliza kama hatujafikia makubaliano na Serikali, hii miradi ya maji ambayo mingi imeanzishwa tangu kwenye bajeti ya mwaka 2012/2013 mpaka leo miradi ya maji haijafikia hata asilimia 50.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa pia, ninaangalia kwenye ukurasa huohuo, tunazungumzia kwamba, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya kwa mwaka 2016/2020. Ukienda kwenye hoja Kamati ilipendekeza shilingi bilioni 30 ziende kwenye utekelezaji wa ujenzi wa zahanati na ujenzi wa vituo vya afya, lakini hadi sasa Serikali inasema bado haijapata itatumia shilingi ngapi katika utekelezaji wa hiyo miradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana tumepitisha bajeti na tunaendelea na mwaka huu tena tutapitisha bajeti. Sasa hivi tunavyoongea tuko kwenye robo ya tatu ya bajeti ya mwaka 2016/2017, pesa kule chini zinaenda kwa asilimia ndogo sana. Kwa hiyo, tuombe Serikali iwe sikivu na tunafahamu Serikali yetu ni sikivu, Serikali ya Chama cha Mapinduzi iweze kusikia na kuona ni jinsi gani tunapeleka pesa za maendeleo huko chini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia, nizungumzie zile milioni 50 kupeleka kule vijijini. Ukiangalia kwenye ukurasa wa 11 unaona kwamba Kamati imeshauriana na kukubaliana na majibu wa Serikali kuwa imeridhia shilingi bilioni 59.5 sawa na asilimia 45 ili iweze kutumika katika kupeleka vijijini na kutafuta zile pilot area. Sasa mimi nikawa naangalia hii pilot program hivi ni Wilaya zipi ambazo zimekuwa specifically kwamba zimekuwa ni pilot area kwa ajili ya utekelezaji wa hizi shilingi milioni 50!
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nilikuwa ninaomba, najua kabisa tuna changamoto nyingi, lakini pia nimeona ukusanyaji wa mapato umekwenda kwa kasi. Ukiangalia kuna Mbunge mmoja amezungumzia kwamba, hata polisi imeingilia kwenye upande wa makusanyo. Polisi ina haki ya kuingilia upande wa makusanyo kwa sababu yale makosa yanayofanyika barabarani, polisi ikikusanya ndiyo pesa zinaingia huko katika miradi ya maendeleo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, hatuwezi kubeza jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali yetu, hususan kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani kwa Polisi kukusanya kodi mbalimbali za makosa. Kwa hiyo, niwatie moyo polisi, nimtie moyo IGP, nimtie moyo pia Waziri wa Mambo ya Ndani kwamba aendelee na ukusanyaji huo wa kodi ili tuweze kufanya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kilimo; mwenzangu aliyekaa amesema zaidi ya asilimia 73, mimi ninavyofahamu ni asilimia 82 inajihusisha na suala la kilimo Tanzania, lakini pembejeo zimechelewa huko vijijini. Watu wamelima, watu wamepanda, pembejeo hazijafika. Ukipita vijijini ni malalamiko. Sasa tunajiuliza kama pembejeo zinachelewa, wakulima wataweza kuvuna vipi? Makusanyo ya Halmashauri nyingi nchini zinapata makusanyo yake kupitia mazao mbalimbali yanayolimwa kule vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninaomba sana kwenye bajeti hii inayokuja tuweze kutenga pesa nyingi kwenye Wizara ya Kilimo. Wizara ya Kilimo ni Wizara nyeti, tunalima tumbaku, tunalima pamba, tunalima alizeti, lakini tunahitaji pembejeo za kutosha. Tunahitaji ruzuku iongezwe zaidi kama mwenzangu alivyosema kwenye mbegu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia nchi ya viwanda, lakini hali ya umeme ni mbaya sana. Kwa mfano, mimi naongelea Jimbo langu, katika vijiji 61 nina vijiji vitatu tu vyenye umeme, lakini Wilaya ile ndiyo tunaozalisha michikichi. Tunazungumzia hapa tuanzishe viwanda vya mawese, tunaanzishaje viwanda wakati umeme wenyewe hakuna. Tunafaya sensitization kwa wananchi waone umuhimu wa kulima zao la mchikichi, umuhimu wa kulima mazao mbalimbali ili tuweze kupata raw materials ya kuweza ku-maintain hivi viwanda. Ninaomba pia kwenye mradi, kama alivyozungumza mwenzangu, lile deni la TANESCO lilipwe, tulipe deni la TANESCO ili miradi ya umeme vijijini iendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo pia, tuiombe Wizara husika iweze kupunguza bei. Wananchi wengi walioko vijijini hawana uwezo wa kulipia umeme kama ambavyo sasa hivi wanavyotaka hiyo pesa tuilipie. Naomba Wizara yenye dhamana ione ni jinsi gani itaweza kupunguza bei ya umeme ili basi wananchi waweze kukidhi haja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba pia kuchangia kwenye miradi ya barabara, hali ya huko vijijini tunatofautiana, sisi miundombinu yetu ni mibaya sana. Niombe katika bajeti tuweze basi zile pesa zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya barabara mbalimbali vijijini ziweze kupelekwa ili miradi hii iweze kutekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa nizungumzie suala la TRA (ukusanyaji wa mapato). Najua dhamira ya Serikali ni njema, hali huko chini sio nzuri sana, unakuta mfanyabiashara kwa mujibu wa Sheria ya TRA wanasema ile turn over ya mwaka kama ni less than 14 million hautakiwi kuwa na ile mashine ya kukatia risiti wateja. Lakini kwenye maeneo mengine kama Dar es Salaam unakuta mfanyabiashara ameshafanyiwa assessment na akaambiwa kwamba labda biashara yako ni milioni tisa ndiyo turn over kwa mwaka, lakini bado baada ya miezi miwili wanarudi wanamwambia tukiiangalia biashara yako kwa macho, tunaona kwamba wewe unatakiwa uwe na risiti, aahhaa! Sasa umeshafanya, umemkadiria, umeona kwamba yuko less than 14 million. Kwa nini tena urudi umwambie kwa macho tu…
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Kamati ya Bajeti kwa Taarifa yao nzuri, ahsante.