Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais ambayo imesheheni kila kitu, matatizo yetu yote yako pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kutoa maneno ya shukrani. Kwanza niishukuru Serikali, tumekuwa tukipiga kelele juu ya uanzishwaji wa Jimbo jipya la Ulyankulu pamoja na Halmashauri na Wilaya ya Ulyankulu. Tunaishukuru sana Serikali, niombe Serikali ikubali shukrani zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, niwashukuru wapiga kura wa Jimbo la Ulyankulu kwa kuniamini. Hawa jamaa kule kwangu wanajua, Mheshimiwa Rais alipata 81% na mimi kwa sababu nilimpigia kelele sana yeye nikapata 75%. Kwa hiyo, hawa jamaa wacha watoke sisi tuendelee na kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishukuru familia ya Mtemi Mirambo. Mwenyekiti wewe ni Mtemi na mimi nikuarifu tarehe 28 Novemba, nimepewa Utemi kwa maana ya kuongoza jamii ya Wanyamwezi wote wa Ulyankulu. Kule kwetu ukipewa Utemi unapewa na jina lingine. Sasa jina nililopewa linatuletea taabu, nimepewa jina la Mbula maana yake mvua, toka siku naapishwa kupewa Utemi mvua zinanyesha siyo kawaida. Itabidi nirudi kwa familia ya Mirambo inioneshe namna ya kuipunguza mvua. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze sasa na mambo mbalimbali yanayotukabili ndani ya Jimbo letu jipya la Ulyankulu. La kwanza, inawezekana watu mkashangaa, bado uchaguzi wa kata tatu haujafanyika ndani ya Jimbo kwa maana ya Kata ya Milambo, Kanindo na Igombe Mkulu. Eneo hili lilikuwa la wakimbizi waliokuja mwaka 1972. Tulikuwa nayo makambi matatu makubwa kwa maana ya Ulyankulu, Mishamo na Katumba. Wenzetu wa Mishamo na Katumba baada ya kupewa uraia wamefanya uchaguzi wa Rais, wa Mbunge pamoja na Madiwani lakini eneo hili la kata hizi tatu wameweza kuchagua Mbunge pamoja na Rais. Niiombe tu Serikali na hasa kwa kuzingatia ahadi za Mheshimiwa Rais alipokuja, kata hizi zifanye uchaguzi haraka iwezekanavyo ili kazi za maendeleo ziweze kufanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini liko tatizo la uanzishwaji wa mamlaka ndani ya eneo lililokuwa Kambi ya Wakimbizi. Kwa hiyo, Serikali tuiombe iharakishe lakini pia Wizara ya Mambo ya Ndani iharakishe kwa sababu ndani ya kambi kwa maana ndani ya eneo hili wapo wakimbizi ambao walikubali kuwa raia, wapo wakimbizi waliokubali kurudi Burundi lakini wapo wakimbizi ambao hawakutaka lolote. Serikali iwaamulie mapema ili jambo hili likae vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, iko shida ndani ya mambo haya, wapo viongozi wa Wizara na hasa Wizara ya Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Kitwanga nadhani utanisikia vizuri, leo anakuja Naibu Katibu Mkuu labda, siwezi kujua kama ni huyu wa sasa, anasema marufuku kujenga, kesho anakuja mwingine anasema pako vizuri. Ifike mahali Serikali inyooshe maneno kwamba lipi linafanyika. Kwa hiyo, nadhani hilo ni vyema tuliweke sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikumbushe tu ahadi ya Rais, pamoja na azma hii ya kubana matumizi, bado iko haja ya kuanzisha Wilaya ya Ulyankulu na Halmashauri yake ili kusogeza huduma. Kutoka Ulyankulu kwenda Kaliua ni mbali, kutoka pale kwenda Kahama kuna kilometa kama 80 lakini kutoka Ulyankulu kwenda Makao Makuu ya Mkoa kuna kilometa 90. Kwa hiyo, niombe tuharakishe uanzishwaji wa Wilaya pamoja na Halmashauri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya ujumla, liko tatizo la maji na Waheshimiwa Wabunge wengi wamesema. Upo mradi unataka kutoa maji kutoka Ziwa Viktoria kupeleka Tabora, Sikonge na Igunga. Kutoka Tabora Mjini kwenda Ulyankulu ni kilometa 90. Niombe sana Serikali ituongezee sisi ili tuwe sehemu ya mradi wa maji ya Ziwa Victoria. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini upo mradi wa maji kutoka Malagarasi kuja Kaliua na Urambo. Kutoka Kaliua kwenda Ulyankulu kilometa 60, sidhani kama Serikali inaweza kushindwa kuunganisha wapiga kura wangu hawa wanaotaabika na shida ya maji. Iko option nyingine, sasa hivi Mto Igombe umejaa kweli kweli mpaka kuna mafuriko, kwa nini Serikali isivune maji yale ambayo yanaweza kutosheleza Jimbo zima na tuka-supply maeneo mengine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la barabara. Tunayo matatizo, barabara kutoka Tabora kwenda Ulyankulu, kama nilivyosema kilometa 90, ndiyo inayotegemewa kuleta tumbaku Tabora kabla haijapelekwa Morogoro. Niombe sana, barabara zote zinazoingia Mji wa Tabora zina lami na kama hazina lami ziko kwenye mpango, Serikali iingize kwenye Mpango huu barabara ya kutoka Tabora kwenda Ulyankulu kujengwa kwa kiwango cha lami. Tutafurahi sana watu wa Ulyankulu, tumechelewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini iko barabara inatoka Ulyankulu kwenda Kahama, kwenye Ilani ya Chama chetu barabara kutoka Mpanda - Kaliua, Ulyankulu - Kahama kilometa 428 iko kwenye Mpango. Mimi niombe sana haya mambo ya kuweka upembuzi yakinifu basi ifike mwisho barabara ianze kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la tumbaku, tutapiga kelele sana na Mheshimiwa Mwigulu umetuahidi tunaotoka kwenye maeneo yenye kilimo cha tumbaku tukutane. Ninachotaka kusema kila Serikali imekuwa inajaribu lakini haifanikiwi. Wakulima wetu wanadhani tunaogopa wazungu wa makampuni kwani watu hawa wanaungana kuwanyonya wakulima wetu. Iko mianya mingi zao la tumbaku linanyonywa. Kwa hiyo, Serikali ifike mahali tukae vizuri turekebishe jambo hili na mambo yaende vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme vijijini, Mheshimiwa Muhongo, umeme unaotoka Tabora kwenda Ulyankulu mradi huu unasuasua. Wenzetu wa Upinzani wakati wa kampeni walisema zile nguzo tutatengeneza mkaa. Sasa zimelala chini, sehemu kubwa kazi ile haijafanyika. Niombe tuongeze speed ili wananchi waamini kweli kuna umeme unakuja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, liko tatizo la maslahi ya Madiwani. Waheshimiwa Wabunge, tunapokuwa kwenye kampeni Madiwani wanatupigania sana na mara nyingi tunasema mafiga matatu, hakuna maslahi mazuri kwa Waheshimiwa Madiwani, watu ambao wanafanya kazi kwa niaba yetu. Madiwani wanalipwa kidogo lakini pia hawaheshimiwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nizungumzie kipindi ambacho Madiwani wanakuwa hawapo wamekwenda kwenye uchaguzi, kazi zile hufanywa na watendaji wa Halmashauri kwa maana ya Wakuu wa Idara. Mwezi Novemba, Katibu Mkuu TAMISEMI, najua ameshaondoka lakini Serikali ipo, alitoa Waraka wa ajabu sana. Naomba nisome kipengele kimoja kwa ruhusa yako halafu uone jinsi gani tunawanyima Waheshimiwa Madiwani kazi.
MWENYEKITI: Ahsante sana Mtemi.
MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.