Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nitangulize shukrani zangu za dhati kwa Serikali yangu ya CCM. Nampongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri wa Fedha na Sekretarieti yake kwa kuthubutu kutoa mapendekezo yao kwa Mpango huu wa Maendeleo wa Mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, mapendekezo haya ni mazuri kwa sehemu kubwa. Mchango wangu katika mapendekezo yangu upo katika sehemu tatu:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni Elimu ya Bure Shule za Msingi na Sekondari. Kwa maoni yangu, fedha hizi zinazotolewa mashuleni na hasa shule za msingi, hazifanyi kazi iliyokusudiwa. Mfano, Shule ya Msingi „A‟ kwa mwezi itapata shilingi 230,000/=. Fedha hizi hugawanywa kwa asilimia ishirini ishirini. Kwa maoni yangu, fedha hizi hazitoshi hata kununua mpira.
Kwa mahitaji makubwa ya shule ni chaki, mitihani na utawala. Kwa nini Serikali isifungue akaunti maalum kila Halmashauri na fedha hizi zikawa katika akaunti hii na kila shule ikapewa mahitaji muhimu ya wanafunzi na utawala. Napendekeza style iliyokuwa inatumika enzi za Mwalimu, kila mwanafunzi alikuwa anapewa vitabu, madaftari, chaki na vitu vingine muhimu kuliko fungu la fedha hizi ambazo sehemu kubwa hazifanyi kazi. Fanyeni utafiti.
(b) Nashauri Serikali itenge fidia ya wakulima kwa mazao yaliyoharibiwa na wanyama waharibifu (ndovu) Jimboni kwangu. Wakulima wanadai zaidi ya shilingi milioni 400. Serikali ihakikishe fidia kwa wakulima, inalipwa.
(c) Malambo kwa wafugaji. Maeneo mengi ya hifadhi ya Taifa hayana maji kwa mifugo. Serikali iwe na mpango maalum wa kuchimba malambo Jimbo la Bunda.
(d) Vile vile Serikali iwe na mpango maalum wa kujenga vyumba vya madarasa, vyoo na nyumba za Walimu kwa shule za msingi na sekondari. Mfano, Jimbo langu la Bunda lina upungufu wa vyumba vya madarasa 586 vyenye thamani ya shilingi milioni 687. Serikali iwe na mkakati maalum wa kujenga/kutatua kero hii.