Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kilimo halijapewa kipaumbele, limezungumzwa kidogo sana katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2017/2018. Ni vema kilimo kikapewa kipaumbele ili pia kufikia nchi yenye viwanda tunayoiota. Karne ya 18 na 19 mwanzoni, nchi ya Uingereza ilifanya mapinduzi makubwa sana ya kilimo (Agrarian Revolution) na ndiyo matokeo ya viwanda vya Uingereza vilivyopo hadi leo. Vivyo hivyo nchi za China na India zote zilifanya mapinduzi ya kilimo (Agricultural Revolution) na hatimaye zikafikia hatua ya kuwa na viwanda ambavyo vipo hadi leo. Hivyo hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kufikia mapinduzi ya viwanda bila kuboresha kilimo.