Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza sina budi kumshukuru Mungu kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kuchangia hoja hii ya Fedha na Mipango.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bandari ya Dar es Salaam. Ni bandari ambayo inaipatia pato Serikali yetu kwa kiasi kikubwa, lakini leo hii tunakosa mapato makubwa kutokana na kodi kubwa kuongezeka na wafanyabiashara kukimbia bandari yetu kwa kuogopa kula hasara. Wafanyabiashara wa Congo, Zambia, Malawi, wote hao wamekimbia na kuifanya Bandari kuwa kavu. Kuna upungufu wa makontena, magari ya mizigo hayaingii, wengi wamekosa ajira na uchumi kudorora.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge kazi yetu ni kuelekeza Serikali na kuishauri na kuikosoa pale inapofanya vibaya na kuisifu pale inapofanya vizuri. Sasa umefika wakati wa Mawaziri kusema ukweli, wasimdanganye Mheshimiwa Rais kwa kuogopa kutumbuliwa, hii ni nchi yetu sote, Watanzania wanatutegemea, tunakokwenda siko. Uchumi unaporomoka kutokana na mipango mibovu kuanzia matajiri mpaka mama ntilie. Mheshimiwa Waziri tunakwenda wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Tano, kipaumbele chake inajipanga kufufua viwanda na kujenga viwanda, lakini haiwezi kufanikiwa ikiwa miundombinu ya umeme na maji ni mibovu, ni lazima kwanza ijipange. Serikali kwa kusimamia kupatikana kwa umeme wa uhakika ili wanapokuja wawekezaji kuingia nao mkataba waweze kufanya kazi na kuipatia nchi uchumi na vijana wetu kupata ajira na kupatikana maendeleo. Porojo za kwenye makaratasi hazitoshi tufanye maamuzi ya kiutekelezaji ndiyo dira ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu ya umeme wa uhakika inaweza kuendesha viwanda na kukidhi matumizi mengine ya wananchi wa kujikwamua kimaisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo bado hakijapewa kipaumbele kwani benki hazitoi mikopo ili miradi ya kilimo iendelee; ni usumbufu mkubwa. Pembejeo hakuna, vitendea kazi kama vile matrekta, mbegu bora hakuna za kutosha, hivyo wakulima wapate mbolea mapema na bei zipunguzwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, vyanzo maji vya vingi vimekauka kutokana na uharibifu wa mazingira na ukataji wa miti hovyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Waziri atatuambia nini kuhusu upatikanaji wa mikopo ya fedha kutoka benki ili wakulima waweze kufaidika kwa kupata mahitaji yao ili kukuza uzalishaji na kupunguza umaskini?
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango wangu huu, naomba kuwasilisha.