Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mchuchuma na Liganga. Suala la mradi wa madini ya Mchuchuma na Liganga limechukua muda mrefu, naiomba Serikali sasa ichukue hatua haraka ya kutatua tatizo la kulipa fidia kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya madini ambapo waliahidiwa kulipwa mwezi Juni, 2016, kiasi cha Shilingi bilioni 14. Pia Serikali ikamilishe mazungumzo kuhusu bei za umeme ambayo inasuasua. Wananchi wamehamasishwa kulima matunda na nafaka kwa kutegemea kupata soko la uhakika kwenye machimbo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Utawala Bora. Wafanyakazi/watumishi wengi wa umma wanafanya kazi kwa hofu na woga na kupoteza ubunifu kutokana na utumbuaji wa majipu ambao haufuati utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wakubwa kwa wadogo wamekata tamaa sana kutokana na kodi zisizo na utaratibu, TRA inawakamua sana wafanyabiashara hao. Wafanyabishara wadogo wananyanyaswa sana kwa kutozwa kodi nyingi na hata kuua mitaji ya wafanyabiashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, Miundombinu. Tunapoongelea suala la Liganga na Mchuchuma lazima suala la barabara lipewe umuhimu sana. Barabara ya Njombe Mjini – Ludewa ni ya vumbi na kipindi cha mvua inaharibika sana. Naomba barabara hii iingie kwenye mpango wa 2017/2018 kwa ajili ya maandalizi ya uchimbaji wa madini ya Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Maji; gharama za maji zinawatesa wananchi, naomba suala la maji na gharama za maji ziangaliwe, wananchi wanaletewa bili kubwa za maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na naomba kuwasilisha.