Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ANATROPIA L. THEOPIST: Mheshimiwa Naibu Spika, Kuondoa Milolongo ya Vikwazo Katika Uwekezaji; mlolongo wa utaratibu wa kumiliki ardhi ni gharama kubwa ya upimaji na umiliki wake. Wingi wa Tozo mbalimbali, kodi na ushuru katika biashara na huduma ziwe harmonized na zipunguzwe ili kuvutia zaidi uwekezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuandaliwe vipaumbele vichache vyenye kuandaa mazingira ya uchumi wa viwanda na kuhakikisha vinatekelezwa. Kwa mfano mpango ujao uhakikishe fidia zinalipwa kwa ajili ya EPZA kwa angalau asilimia 60 na Miradi ya Chuma na Umeme tu, tofauti na mpango unaoonesha vipaumbele zaidi ya 16, katika nchi yenye uchumi mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipaumbele kingine kuelekezwa iwe katika kilimo ambayo ndiyo sekta inayoajiri watu wengi. Hii iende sambamba na uanzishaji wa viwanda vidogo vidogo vya kuhudumia au kuongeza thamani katika mazao yao. Hii iende sambamba na kuongeza pesa katika taasisi zinazounda viwanda hivi kama TEMDO, COSTECH, TIRDO etc.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuongeza ushirikishaji wa sekta binafsi kati maandalizi ya sera, kodi na tozo mbalimbali. Kwa mfano, kuanza kutoza asilimia 18 kwenye auxiliary services za bandari na katika sekta ya utalii imepelekea anguko kubwa la kibiashara kwani wahusika hawakuwa wamejiandaa kwa mabadiliko husika, hali kadhalika wasafirishaji, TATOA, TAFFA na wadau wengine wanaohusika na upandishaji wa tozo hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ubunifu Katika Kuibua Vyanzo Vipya vya Mapato. Kumekuwepo na changamoto ya kodi mpaka kuwa kero. Ubambikaji wa kodi toka kwa maafisa wa TRA kwa lengo la kuongeza pato la ndani, ikienda sambamba na focus kwa makosa ya barabarani ni mzigo unaobebwa na watu wachache tu. Wizara na Serikali iwaze vyanzo vipya vya kodi ili kodi isambae na isiwe mzigo kwa watu wachache kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuwe na mpango wa kuoanisha elimu na uchumi wa viwanda tunaouendea, kuandaa wanafunzi sambamba na tunakotaka kwenda, tofauti na ilivyo sasa ambapo wanafunzi hata wakimaliza vyuo hawana ujuzi wa kile kinachohitajika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kusambaza Uchumi; Mipango ioneshe dhahiri yale maeneo yaliyosahaulika kama vile Mikoa ya Kagera, Mwanza, Kusini na mengineyo inayosadikiwa kuwa maskini ili ipewe kipaumbele katika miradi ya maendeleo. Hatutarajii kuona mchanga unaongezwa kwenye kichuguu, Priority has to be to less developing regions
Mheshimiwa Naibu Spika, kuwe na mkakati thabiti wa kutekeleza bajeti ambazo tumekuwa tukiziandaa kila mara. Kwa mfano, bajeti zimekuwa zikiletwa Bungeni lakini mpaka mwisho wa mwaka pesa zinakuwa hazijapelekwa. Tunatarajia kuona namna ambayo pesa zitapatikana na si tozo na kodi kero tunazoziona kwa sasa.