Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ni ya viwanda, napenda kushauri katika Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2017/2018, sekta ya kilimo ipewe kipaumbele cha kwanza ili kuwezesha pembejeo za kilimo kupatikana kwa wakati na itengwe bajeti ya kutosha. Kwa kufanya hivyo, wananchi watalima mashamba ya mazao ya biashara na chakula na kuwezesha viwanda vyetu kukua kwa kasi na kuinua uchumi wa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya maendeleo ili iweze kwenda na wakati ni lazima fedha za miradi zinazopitishwa na Bunge lako Tukufu zipelekwe kipindi husika. Angalia bajeti mwaka 2016/2017 hadi robo ya mwaka hata senti tano ya miradi ya maendeleo hazijapelekwa kwenye Majiji, Manispaa, Halmashauri na Miji Midogo.