Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, namshauri Waziri aangalie upya ongezeko la kodi eneo la mapato ya ndani. Kila mwaka tunapoongeza budget projection ya nchi matokeo yake kila biashara inaongezewa kodi. Kuongezeka kwa kodi katika biashara ileile, mtaji uleule na mauzo yaleyale au yaliyopungua kwa zaidi ya asilimia 50, kunasababisha wafanyabiashara wengi kushindwa kulipa kodi, kufilisika na kufukuza wafanyakazi. Serikali iangalie vyanzo vipya kama kuanzisha malipo au tozo kwenye pikipiki zote kwa kuwa wanaoziendesha siyo wamiliki wake. Kuruhusu biashara hiyo kuwa bure maana yake wapo matajiri wengi hawalipi kodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali iongeze uwekezaji katika kilimo cha mazao ya biashara na chakula. Kwa kuwa kama wananchi watawezeshwa vizuri katika kilimo tatizo la fedha litapungua.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iweke mpango mahsusi kuhusu maji. Mpango huo uhusishe ongezeko la Sh.50 kwenye lita ya mafuta ambayo yanaingia nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa ulipaji wa Road Licence uwe tofauti na sasa na nashauri kodi hiyo iunganishwe kwenye bei ya mafuta ambapo kila lita moja iwekewe ushuru maalum wa mafuta kulipia kodi hii. Mfano gari moja linatumia lita 20 kila siku zidisha kwa mwaka mmoja (20x360=7,200 lita). Ukichukua lita 7,200x50% tu ambayo itaongezwa kwa gari ndogo (tax) italipa ushuru wa Sh.360,000. Ushauri wangu hapa ni kwamba Road Licence fixed ikiondolewa na kuwekwa kwenye mafuta Serikali itapata pesa nyingi zaidi.