Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naunga mkono Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2017/2018, pamoja na kutofahamishwa rasmi mafanikio na upungufu wa utekelezaji wa mwaka 2016/2017 hadi sasa ili kutupa picha kwa mapendekezo ya mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeweka asilimia 40 ya bajeti kwa maendeleo lakini hadi sasa fedha hizo hazijafika kwenye Halmashauri zetu na kupelekea kuzorota kwa utekelezaji wa maendeleo kwenye huduma za jamii kama afya, maji na umeme. Nashauri katika kipindi hiki, kabla ya kufika mwaka 2017/2018, kuboresha mwenendo wa usambazaji wa fedha za maendeleo kwa angalau asilimia 75 kwa miradi ya maji, afya na umeme kwani huduma hizi zinawagusa wananchi wengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kusonga mbele na kuendelea kuweka mazingira ya malalamiko kwa baadhi ya viongozi na wananchi kwa maendeleo yao kiuchumi, nashauri Serikali kujikita zaidi kujenga mikakati ya kufufua mazingira bora ya kilimo, biashara na fursa za ajira binafsi kwa vijana wetu. Pia kuwepo na uratibu wa malalamiko na kuyapanga kwa utekelezaji ili kuepusha malalamiko kujirejea ndani ya mipango yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono mapendekezo haya ya Mpango wa mwaka 2017/2018.