Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia kuhusu Annual Motor Vehicle License. Nashauri Serikali katika Mpango wake iangalie namna ya kurekebisha sheria hii ili isiwaumize wanaomiliki vyombo vya moto na wale wanaouza vyombo vya moto. Aidha, Serikali iweke katika Mpango wake namna ya kusamehe malimbikizo ya kodi hiyo kwa watu waliouza vyombo vya moto kama pikipiki halafu waliouziwa hawakubadilisha umiliki.