Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viwanda vya kukuza uchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda, ukurasa wa 52, 6.3(e), nashauri iongezeke mafuta ya mawese. Tanzania inaagiza mawese tani 600,000 kwa mwaka inayogharimu dola milioni 450 ya fedha za kigeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Kigoma unaweza kuzalisha zaidi ya kiwango hiki iwapo wananchi watahamasishwa kulima michikichi na kuvutia uwekezaji kwenye viwanda vya mazao ya mawese. Manispaa ya Kigoma inahamasisha mfumo wa one family, 1hc ili kuzalisha tani 80,000 za CPO.
Mheshimiwa Naibu Spika, marekebisho, page 52 ya mapendekezo, barabara hii inapaswa kuitwa Manyovu-Kasulu-Kibondo-Kabondo na siyo kama ilivyoandikwa. Nashauri muwasiliane na Wizara ya Uchukuzi maana kuna mabadiliko kwenye jina la mradi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pongezi, page ya 18, tafsiri ya Reli ya Kati imetolewa vizuri. Ni sawa sasa, hii ndiyo tafsiri sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukurasa wa 43, kilimo cha mpunga. Katika Mkoa wa Kigoma, Manispaa ya Kigoma-Ujiji kuna mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika delta ya Mto Lwiche. Mradi huu unatarajiwa kufadhiliwa na Mfuko wa Falme ya Kuwait (Kuwait Fund) kwa gharama ya dola milioni 15. Hata hivyo, Serikali ya Tanzania inapaswa kutoa fedha za feasibility study na detailed design. Naomba mradi huu mkubwa sana wa hekta 3,000 uingizwe kwenye orodha ya ukurasa wa 43. Pia naomba upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umalizike ili tuweze kupata mradi huu ndani ya 2017/2018.