Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Naibu Spika, malengo makuu (objectives) ni matatu badala ya manne. Lengo la nne lililotajwa kama ufuatiliaji si sawa, hii ni 4001 ya kufuatilia utendaji kazi ili kufuatilia malengo tajwa, page one.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya kipaumbele kwa mwaka 2017/2018 kunakosekana the main priorities, page 18-22 ya hotuba ya Waziri. Maeneo tajwa ni 39, ni mengi mno kuweza kufanikisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, the concept (dhima) ni kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na maendeleo ya watu. Hali halisi ya kiuchumi, je, tumefanikisha kwa kiasi gani dhana ya kilimo ni uti wa mgongo? Focus ya uchumi wa viwanda ni ipi? Ni rasilimali gani zinalengwa kwa aina gani ya viwanda? Kuna rasilimali watu inayolengwa maalum kwa aina gani za viwanda? Je, ni masoko gani yanayolengwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango unatakiwa kuainisha main strategies zitakazowezesha kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi. Mfano, ni maeneo gani makuu matatu Serikali inatakiwa ku-focus into ili kusukuma maendeleo katika sekta nyingine?