Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia. Pamoja na kuleta Mpango wa Maendeleo wa 2017/2018 napenda kujua ni kwa kiasi gani mpango wa 2016 uliweza kutekelezwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya uchumi kwa maelezo ya Waziri inaimarika, lakini kwa uhalisia hali ni mbaya katika sekta nyingi. Mfano benki nyingi za biashara mikopo imeshuka na riba ni kubwa hata vyombo vya habari vimenukuliwa vikisema hayo. Baadhi ya benki mfano CRDB imepata hasara ya shilingi bilioni mbili na zaidi. Wafanyabiashara wanashindwa kurudisha mikopo na wengi wao hawaagizi tena bidhaa kutoka nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata Serikali yenyewe kwa mwaka 2016 akiba ya fedha za kigeni ilifikia dola milioni 3,870.3 na hizi zinaweza kuagiza bidhaa nje kwa miezi minne. Je, baada ya miezi minne Serikali imejipangaje? Thamani ya Tanzanian shilling inazidi kushuka na deni la Taifa linazidi kukua, hii ni hatari sana kwa Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya viwanda; Serikali imekuwa ikiimba wimbo wa nchi itakuwa ya viwanda, je, kuanzia wakati wa kampeni hadi sasa ni viwanda vingapi vimeongezeka? Bila kuwa na umeme wa uhakika na kilimo cha kibiashara ili wazalishe, viwanda hivyo vitakuwa ni vya nini? Tulikuwa na kiwanda cha General Tyre Arusha kilichobinafsishwa na Serikali ikakichukua na imekuwa ikitoa ahadi zaidi ya miaka kumi kiwanda kitaanza kazi lakini mpaka leo hakuna uelekeo. Ikumbukwe kiwanda kile kilikuwa kinazalisha matairi bora na kutoa ajira nyingi na Serikali kupata mapato. Nilitegemea Serikali ingetueleza ina mpango gani na kiwanda kile.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Utalii; hii ni kati ya sekta inayochangia katika pato la Taifa kwa zaidi ya 17%, lakini kwa sasa Serikali inaelekea kwenda kuua kabisa utalii katika nchi yetu. Kitendo cha Serikali kuongeza VAT katika utalii ukizingatia tayari sekta hii ina zaidi ya kodi/leseni 31 zinazolipwa, utalii wetu umekuwa ni ghali sana. Sipingi kulipa kodi lakini tupandishe kwa taratibu. Baadhi ya nchi za Ulaya sheria zao huwezi kupandisha bei zaidi ya 10%. Hivi hawa tembo, simba, twiga na kadhalika kutoka Tanzania tumewaongezea thamani gani wawe na bei kubwa kuwaona kuliko wale waliopo nchi jirani ya Kenya ambao hawalipiwi kodi?
Mheshimiwa Naibu Spika, ningetaka kujua hivi Wizara ya Fedha inapoandaa Mpango ni kwa kiasi gani wanashirikiana katika mawazo ya kupanga hii mipango na Wizara nyingine? Hivi inapoanzisha viwanda ni kwa kiasi gani wameandaa wataalam, malighafi na kadhalika?