Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, tunajadili mapendekezo ya Mpango wa Bajeti ya mwaka 2017/2018 huku Serikali ikiwa haijatoa fedha za maendeleo kwa ajili ya miradi kwenye halmashauri na wilaya kwa sehemu kubwa na hivyo kusababisha miradi kudorora.
Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Waziri wa Fedha inaonesha wastani wa pato la kila Mtanzania ilikuwa sh. 1,918,928/= sawa na USD 96.5 mwaka 2015.
Hizi takwimu haziendi na hali halisi ya wananchi wengi zaidi ya 809 wanaoishi vijiji ambao hawana uwezo wa kupata hata 100,000 kwa mwezi. Wengi wanapata mlo mmoja tu kwa siku. Serikali itueleze ni maeneo gani ya nchi yetu ambapo takwimu hizi zinatolewa/zinachukuliwa ambapo hazitoi hali halisi za maisha ya watu wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ongezeko la watu ndani ya nchi yetu ni kubwa sana haliendani na uwezo wa Serikali kutoa huduma muhimu na za uhakika. Ikiwa sensa ya mwaka 2012 tulikuwa watu milioni 45 mwaka 2016 tunakadiriwa watu milioni 50.1 na mwaka 2025 tutakuwa milioni 63 hii ni hatari kwa ustawi wa watu wa Taifa letu. Kwa mikakati gani ya Serikali kudhibiti ongezeko na kasi kubwa ya ongezeko la watu kwa nini Serikali inanyamaza kimya wakati inaona hatari iliyoko mbele?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Serikali ihakikishe kipengele cha kufungamanisha maendeleo ya uchumi na maendeleo ya watu kinatekelezwa kikamilifu; mpango wa elimu bure umesaidia kupunguza machungu kwa wazazi na watoto wengi kuandikishwa mashuleni, bado fedha inayotolewa ni kidogo haitoshelezi mahitaji ya watoto na shule zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mpango ujao lazima Serikali iongeze fedha ya capitation zinazopelekwa mashuleni baada ya kufanya tathmini na kutambua mahitaji ya wanafunzi ili wapate elimu nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwenye mpango ujao ilete mpango kamili wa kujenga vyuo vya mafunzo ya ufundi (VETA) kwenye Wilaya zote hapa nchini ambazo hazina mahitaji ya vyuo vya VETA, ni muhimu sana kwa ajili ya kujenga stadi za kazi kwa watoto wanaofeli wanaokosa nafasi ya kujiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine vya mafunzo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka mpango ujao uoneshe mikakati ya kujenga zahanati kila kijiji na vituo vya afya kila kata ili kuokoa maisha ya watu yanayopotea kwa sababu ya huduma za afya kuwa mbali na watu. Njia pekee ya kupunguza vifo vya watoto na wanawake, wazee na makundi mengine ni kutotekeleza mpango wa kupeleka huduma hizi jirani na wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji wa maji safi na salama; tatizo la ukosefu wa maji ni kubwa sana linazidi kukua kutokana na ongezeko kubwa la watu. Mpango wa mwaka 2017/2018 lazima Serikali ioneshe mkakati wa kuondoa tatizo la maji, miradi mikubwa ya maji, Mkoa wa Tabora kutoa maji Ziwa Victoria, mradi wa maji kutoka Malagarasi kwenda Kaliua na Urambo na miradi yote ya kimkakati katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikopo ya elimu ya juu; mpango ujao kwanza tathmini ya uhakika ifanyike kuanzia mashuleni na vyuoni ili kubaini mahitaji halisi/wanafunzi wanaohitaji kunufaika na mikopo hiyo ili kutenga fedha za mikopo ya elimu ya juu kuendana na mahitaji na kuwezesha watoto wa maskini kupata elimu mpaka vyuo vikuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa mapato yote ya Serikali kuingizwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali kufuta utaratibu wa retention uangaliwe kwa mapana. Lisipoangaliwa vizuri kuna taasisi na mashirika ya Serikali yataathirika sana – mashirika yanayojiendesha yenyewe bila ruzuku ya Serikali na yanalipa kodi zote stahiki na asilimia zilizoelezwa na Serikali mfano mashirika ya uhifadhi mfano TANAPA, Ngorongoro, TAWA, TFS, NHC.