Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri na timu nzima ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuja na mpango ambao unatekeleza ule mpango wa miaka mitano, Mpango wa Maendeleo endelevu na ilani ya CCM. Nipongeze mambo yafuatayo ambayo ni makusanyo yameongezeka na udhibiti wa matumizi umeongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara iangalie kwa makini changamoto zifuatazo:-
Ukusanyaji wa kodi wenye ufanisi na matatizo ya ukusanyaji kwa maofisa na walipa kodi. Uwekezaji sekta binafsi kumudu ushindani wa bidhaa nje unaotokana na “application ya VAT; cash flow management, mzunguko wa fedha (money supply), ukuaji wa uchumi na hali halisi ya maisha, kupeleka fedha za bajeti zilizotengwa na kwa wakati.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, Serikali iendelee kupanua wigo wa ukusanyaji, mkazo uwe pia kwenye makato yasiyo na kodi (non-tax revenue) hususan taasisi zilizo chini ya TRA. Tuangalie namna kodi (VAT) itakavyowalinda sekta binafsi, tuangalie mnyororo wa huduma, mfano tuwezeshe kilimo chenye tija, kilimo kitoe malighafi za viwanda tujenge viwanda ambavyo ni soko la viwanda vyetu. Kilimo na viwanda vitainua uchumi na kuleta ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iangalie vizuri utekelezaji accounting framework ya “accrual basis of accounting ili tuweze kuwa na cash ya kutosha mwanzoni mwa mwaka miradi isisimame mwanzoni mwa mwaka. Uwepo uhakiki wa data “data integrity” ili consumer price index” ijengwe kwa kuzingatia mtawanyiko wa masoko.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii itawasaidia menejimenti ya real economy na Nominal economy ili kuondoa dhana ya ukuaji uchumi na hali halisi. Program based on budgeting inayolenga kuanza na Wizara nane itayarishwe kwa makini kwani inahitaji taarifa nyingi, inataja kuwa na “activity” nyingi, ngumu sana kuainisha shughuli (activity) na matokeo lengwa/malengo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono mpango huu.