Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango huu haujaonesha baadhi ya sekta katika kukuza pato la Taifa:-
(i) Sekta ya madini
(ii) Sekta ya Maliasili na Utalii
(iii) Bandari
(iv) Gesi
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kufahamu sekta ya madini itachangia kiasi gani? Hisa za Serikali katika miradi ya uchimbaji madini kwenye migodi ya Geita, Mwadui, Buzwagi, Tanzanite One na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika nchi yetu, uchimbaji wa gesi umeanza lakini katika mpango huu haujaonyesha ni kwa namna gani sekta hii itaongeza pato la Taifa. Pia ningependa kujua ununuzi wa vitalu mpaka sasa ni vitalu vingapi viko mikononi mwa wawekezaji na vinaingiza shilingi ngapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huu haujaonyesha sekta ya maliasili ina malengo kiasi gani. Napenda kujua mchango wa Serikali katika mpango huu wa 2017/2018. Kwenye upande wa Bandari pia uko kimya ni kwamba Bandari ndiyo inakufa?
Mheshimiwa Naibu Spika, ili tufike kwenye Tanzania ya viwanda ni lazima tuwekeze kwenye kilimo na siyo kilimo tu. Tunahitaji kilimo cha kisasa ili tuwe na malighafi kwa ajili ya viwanda. Pia kwenye mpango huu kilimo alichokitaja Mheshimiwa Waziri upande wa mazao ni mazao ya chakula tu. Ushauri wangu, tuongeze mazao ya biashara.
Mheshimiwa Naibu Spika, Afya; ndani ya nchi sasa madawa yamekuwa tatizo, tusipoongeza fedha upande wa afya ni dhahiri kuwa katika viwanda tunavyotarajia kuvijenga tutaendelea kuajiri watu toka nje, hivyo tuna kila sababu ya kuboresha hospitali zetu ili tuwe na jamii yenye afya bora.