Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu. Naomba nichangie kwa maandishi katika Mpango wa 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, mizigo kupungua Bandari ya Dar es Salaam; mizigo imepungua kutokana na urasimu au wizi wa mizigo ya wafanyabiashara na kodi kubwa kuliko thamani ya mizigo tofauti na bandari ya Mombasa - Kenya; Beira Port - Mozambique; Durban Cape town na Port Elizabeth za Afrika ya Kusini. Bandari nne za Tanzania ni sawa na mapato ya bandari ya Mombasa, Kenya.
Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri; Mamlaka ya Bandari (TPA) isifanye kazi kimazoea (business as usual) ifanye kazi kiushindani, iondoe urasimu katika utoaji mizigo; mizigo iweze kutolewa katika muda mfupi (min – 24 hours – max 72 hours).
Mheshimiwa Naibu Spika, ili bandari zote za Tanzania zifanye kazi kwa viwango vinavyokusudiwa, mizigo ifanyiwe classification. Aina ya mizigo ya Mikoa; Kanda ya Kaskazini- Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Mara, Mwanza na Kagera, mizigo ishushe katika bandari ya Tanga. Mizigo ya Mikoa ya Kanda ya Kati- Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Tabora, Singida, Shinyanga na Kigoma, mizigo ishushwe katika Bandari ya Dar es Salaam; meli nyingi zinatumia muda mrefu katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, mizigo ya Mikoa ya Kanda ya Kusini (Southern Regions) Mtwara, Ruvuma, Mbeya, Rukwa, na Katavi, mizigo ishushwe katika bandari ya Mtwara. Hii iangalie pia shehena ya mizigo ya Kimataifa na izingatie hali ya kijiografia (Geographical Conditions). Mfano, mizigo ya Burundi, Rwanda, Uganda na Sudan Kusini ishushwe bandari ya Tanga na mizigo ya Malawi, Zambia na Congo, ishushwe bandari ya Mtwara na Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, inatia huzuni kuona au kusikia kuwa katika Bank Economic and Investment Report kuwa, katika nchi 140, Tanzania inashika nafasi ya 120 huku tukiwa na rasilimali na malighafi nyingi tofauti na nchi nyingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, TRA na Mapato; pamoja na taarifa ya ukusanyaji mkubwa wa mapato unaofanywa na TRA, lakini wafanyabiashara wanakamuliwa sana, wanafanyiwa makisio (assessment) makubwa kuliko faida inayopatikana katika biashara zao. Matokeo yake, wafanyabiashara wengi wanafunga biashara zao au viwanda vyao. Wengine wanadiriki kuhamia nchi jirani za Burundi, Rwanda, Mozambique, Uganda, Kenya na Sudan Kusini.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati TRA inaongeza mapato ya Serikali, lakini inaua biashara na kuzorotesha uchumi wa nchi yetu. TRA inakamua ngo‟mbe maziwa hadi anatoa damu bado TRA inakamua tu! Nashauri TRA ifanye utafiti na uchambuzi ili ijue kwa nini wafanyabiashara wanailalamikia TRA na ikibidi itumie Demand Law System.
Mheshimiwa Naibu Spika, Third Law of Demand; in the high price low demand and in the low price high demands. Maana yake, kodi ikiwa kubwa walipaji watakuwa kidogo na kodi ikiwa ndogo walipaji watakuwa wengi. Wahindi wanasema, „dododogo bili shinda kubwa moja‟.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupeleka property tax kukusanywa na TRA ni kuzuia Halmashauri zetu nchini. Je, Mheshimiwa Waziri Mpango, Serikali imeamua kuziua Halmashauri kwa kuwa vyanzo vyake vikuu vyote vinatwaliwa na TRA? Tanga City Council imenyang‟anywa hadi nyumba za kupangisha! Naomba Serikali irudishe property tax itwaliwe na Halmashauri zetu. Tanga City Council irudishiwe nyumba zake na kupangisha. Zipo Serikali za aina mbili, Central Government and Local Government hivyo, tusizinyong‟onyeze Local Government.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ya Viwanda; viwanda vinahitaji umeme wa uhakika, vingi vimekufa au kuuzwa na Serikali. Ushauri; Serikali ifufue viwanda vilivyokufa kwa kuweka mitambo mipya. Mfano, Steel Rolling Mills, Sikh Saw Mill, Kamba Ngomeni na kadhalika katika Mkoa wa Tanga; General Tyres - Arusha; na Kiwanda cha Nyuzi, Tabora.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kilimo, Mifugo, Michezo na Uvuvi vyote vinahitaji kuboreshwa na kutekelezwa kwa vitendo.