Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kuja na mpango huu mzuri wa maendeleo, yapo maeneo ambayo Serikali imefanya vizuri sana:-
(1) Elimu bure licha ya changamoto inayojitokeza. Elimu ya juu hususani mikopo naiomba Serikali itatue changamoto hiyo.
(2) Afya ya mama na mtoto mpango huu umewekwa vizuri sana.
(3) Tulipitisha bajeti ya sh. 50,000,000 kila Kijiji naomba isomeke kila Kijiji na kila Mtaa.
(4) Ongezeko la bajeti ya maendeleo toka trilioni 11.5 mpaka trilioni 13.1 hali hii itatusaidia kuharakisha maendeleo.
(5) Mkakati wa ukusanyaji mapato ikiwa ni pamoja na udhibiti wa upotevu wa mapato.
Naiomba Serikali ipunguze utitiri wa tozo na kero kwa wananchi itawapa unafuu wa kufanya biashara na kuinua pato la Taifa. Serikali iboreshe huduma za maji, afya, umeme, barabara pia na reli.