Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nami niwapongeze Wenyeviti na Wajumbe wote wa Kamati zote mbili kwa kazi nzuri, kwa kweli kazi yao ni kwa ajili ya kuimarisha uwajibikaji na matumizi adili ya rasilimali za umma na hili halina budi kuungwa mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuchelewa kwa upelekaji wa fedha, niseme tu kwamba nafikiri hili ni tatizo la kimfumo kwa sababu kwa sasa kwa kweli chanzo kimoja tu cha fedha (upande wa kodi) ndicho kinachofanya vizuri wakati vyanzo vingine havifanyi vizuri na kama havifanyi vizuri tunapo-disburse kwa kutegemea kilichokusanywa huwezi ukazipeleka kama inavyotakiwa kama vyanzo vingine havifanyi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utoaji wa fedha kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa hasa zile za maendeleo; niruhusu tu niseme kwamba, Serikali kuanzia mwezi Julai mpaka Oktoba tuliweza kutoa Shilingi bilioni 177.3 ambayo ni asilimia 14.3 ya bajeti iliyoidhinishwa. Naomba niliambie tu Bunge lako Tukufu kwamba kuanzia mwezi huu wa Novemba Waheshimiwa Wabunge wategemee mtiririko ambao ni mzuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kulipa deni la PSPF na madeni mengine ya ndani; naomba niseme tu kwamba Serikali inaendelea na uhakiki wa madeni haya. Tulishakamilisha uhakiki wa deni la PSPF na sasa tunaendelea kuweka utaratibu wa kukamilisha uhakiki wa Mifuko mingine yote ili tuweze sasa kutoa ile hati fungani ya Serikali na kuweza kuyalipa na mtakumbuka kwamba tumetenga bilioni 150 katika bajeti hii kwa ajili ya kulipa madeni hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa madeni ya ndani, niseme tu kwamba tumeanza kulipa na nilishaeleza Bunge lako Tukufu kwamba hadi sasa katika quarter hii tumeshalipa shilingi bilioni 187.5 kwa ajili ya madeni ya wakandarasi mbalimbali, wazabuni na madeni ya watumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ukusanyaji wa property tax; naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba hadi sasa TRA haijaanza kukusanya property tax kwa sababu ilikuwa ni lazima kufanya maandalizi ya msingi ya kisheria. Kwa hiyo, kwa mfano kutoa tangazo la Serikali, kazi hiyo imekamilika tarehe 30 Septemba, kuna kuandaa kanuni ambazo zinakamilishwa hivi sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kulikuwa na kuoanisha mifumo mbalimbali ya Serikali – Local Government Revenue Collection Information System na Property Rate Management System na kazi hii imekamilika mwezi Oktoba na sasa TRA imeanza kutoa zile ankara kwa ajili ya kudai property tax kwa kipindi ambacho hakijalipwa. Kwa zile halmashauri ambazo hazitaanza kwenye mfumo huu zilishaelekezwa kuendelea kukusanya property tax kwa utaratibu wa kawaida mpaka hapo zitakapofikiwa na utaratibu wa kukusanywa na Mamlaka ya Mapato.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kushughulikia kesi mbalimbali, TRA imefanya hivyo na hadi sasa Ofisi ya DPP imeshawateua Wanasheria 24 wa TRA kwa ajili ya kuendesha kesi hizo. Pia kufikia Aprili mwaka huu, kulikuwa na kesi 117 ambazo zilikuwa na kodi kubwa tu – bilioni 116 na hizi zimeshughulikiwa. Kati ya Aprili na Septemba kesi 63 zilitolewa uamuzi na kati ya kesi 66 tuliweza kushinda kesi 50.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu TIB; niruhusu tu niseme kwamba, hadi kufikia mwezi Septemba mwaka huu TIB ilikwishatoa notice kwa wateja wake 26 ambao wana mikopo ya karibu bilioni 66, ila kati ya hao wateja watatu ambao wana mikopo ya bilioni 24.7 wamekimbilia mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, yalikuwepo pia madai hapa kwamba TIB walikataa kutoa taarifa za wateja. Nafikiri sio kwamba viongozi wa TIB ni kiburi, lakini sheria inawazuia kufanya hivyo. Kifungu cha Banking and Financial Institutions Act ya Mwaka 2006, section ya 48 under the fidelity and secrecy section, inamzuia mtu yeyote kutoa siri za wateja na kufanya hivyo ni kosa, ukifanya hivyo unatakiwa ulipe faini ya si zaidi ya Shilingi milioni 20 au kufungwa kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote. Kwa hiyo, nadhani hiyo ndiyo sababu ya msingi na si kwamba ni ukaidi wameinyima Kamati hiyo taarifa za wateja.
Mheshimiwa Naibu Spika, ilisemwa pia kuhusu mfumo wa IPSAS Accrual Basis; niseme tu kwamba, Serikali inaendelea kujitahidi kutekeleza mpango kazi ambao una-cover miaka mitano ili kuweza kuhakikisha kwamba Mfuko huu unatumika ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuimarisha usimamizi wa misamaha ya kodi; ni ushauri mzuri na TRA imekwishaanza kuchukua hatua na niseme tu kwamba udhibiti wa misamaha ya kodi umeongezeka na Mameneja wa Mikoa wa TRA wamepewa maelekezo mahususi kuweka kipaumbele katika kudhibiti misamaha hii. Zile kampuni ambazo zilitumia misamaha vibaya, kampuni hizo zilizotajwa kwenye taarifa ya CAG zimeanza kushughulikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimalize kwa kusema kuhusu zile bilioni takribani 99 ambazo zinasemwa zilirudishwa Benki Kuu; hizo zilikuwa ni exchequer issues na sio fedha taslimu ambazo zilirudishwa Benki Kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri nimeeleweka, nakushukuru.