Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nizipongeze Kamati zote na Waheshimiwa Wabunge kwa kujadili taarifa hizi. Kuhusu Wizara yangu katika kitabu cha PAC ukurasa wa 63 mpaka 68 imezungumziwa NDC.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninayo mambo machache ya kuzungumzia kuhusu NDC; niwakumbushe kwamba hili ni shirika la kimkakati lililoanzishwa na Mwalimu mwaka 1965, na katika ujenzi wa uchumi wa viwanda NDC tumeipanga kwamba ile miradi ya kimkakati ndiyo itashughulikiwa na NDC. Kumbe wakati tunahamasisha sekta binafsi kujenga viwanda, miradi ya kimkakati itakuwa inashughulikiwa na NDC.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri kwamba hatujaweka mtaji wa kutosha ndani ya NDC kama ilivyokuwa mwaka 2015, lakini mipango inapangwa kulingana na kila mradi. Kwa mfano, unapozungumzia mradi wa Engaruka, unautambua mradi, lakini huwezi kuuwekea pesa mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kukiri, tunayo miradi mingi kwa sababu NDC kazi yake ni kutambua fursa, kutambua maeneo ambayo wafanyabiashara wa kawaida hawawezi kwenda. Kwa mfano tunapozungumzia Mtwara Corridor, ni kazi yake kuitambua na kuitangaza. Tunapozungumzia TAZARA Corridor, ni kazi ya NDC kuitambua na kuitangaza ili hiyo sekta binafsi, iwe ya ndani au ya nje iweze kuingia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya kipekee limezungumzwa suala la Mchuchuma na Liganga. Nirudie tena, kila mtu anapenda Mchuchuma na Liganga ifanye kazi na Kamati imezungumza maneno mazuri, kwamba hatufanyi maamuzi, wakati wa maamuzi ni sasa na dhamana hiyo iko chini yangu mimi. Nimeagizwa niandike andiko nipeleke kwenye mamlaka na mamlaka itaamua, nililisema mara ya kwanza na Mheshimiwa Deo alinifuata hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, narudia kusema, Mheshimiwa Deo na Waheshimiwa Wabunge, Mchuchuma na Liganga maamuzi yake yanatoka sasa, nitapeleka andiko kwenye mamlaka na mamlaka itaamua na mamlaka inataka Mchuchuma na Liganga iweze kuanza. Kwa sababu Mchuchuma na Liganga ikianza ni kwamba ndiko ile reli ya Mtwara unaweza kuijenga kwa sababu kutakuwa na mzigo mkubwa wa kusomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile tuna potential ya watu 5,000, lakini tuna potential ya kutengeneza megawatt 600 za umeme ambazo haziathiriwi na tabia nchi. Nina uhakika bila kuwa-preempt wanaofanya maamuzi kwamba nitakapokwenda mbele yao na sababu hizo, Mchuchuma na Liganga tutafanya maamuzi na kuondoa mambo mawili, matatu ambayo yamekuwa yakiwafanya watu wasifanye maamuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumzwa suala la General Tyre na niwashukuru Waheshimiwa Wabunge mmezungumza maneno mazuri, mmezungumza maneno mazuri kuhusu UDA.
Mheshimiwa Naibu Spika, General Tyre ninayo mimi; zimeelezwa pesa zilizotumika, mimi ndiye niliyezuia kwamba General Tyre hatuwezi kuendelea kuipa bilioni mbili, mnieleze tunahitaji kiasi gani kuweza kuifufua na kuiendesha. Nimelishikilia mimi, nimeweka timu inafanya survey, watanieleza twende vipi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiwa na uhakika na kitu ambacho nitakifanya General Tyre tutaiendeleza. Tunataka kutengeneza kiwanda cha matairi kwa sababu ndiyo kitakuwa sifa ya nchi hii, tunataka kutengeneza shirika kubwa litakalolipa ushuru mwingi, tunataka kutengeneza shirika kubwa litakalowaajiri watu wengi, lakini tunataka kutengeneza shirika kubwa litakalochochea wakulima wa mpira ili watu wanaolima mpira waweze kupata soko.
Mheshimiwa Naibu Spika, yametajwa mashamba ya mpira yaliyopo Muheza na Morogoro; mvute subira. Kwa sababu tutakuwa na uhakika wa soko la mpira tutakuwa na uhakika sasa wa kuwaambia wananchi waweze kulima zaidi, na mpango wetu sisi ni kuyatumia yale mashamba ya NDC kama nucleus farm na kama road base, lakini tutawahamasisha wananchi watumie outgrowers kuweza kuzalisha mpira zaidi kwa ajili ya viwanda vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo vilevile kwa mradi wa Engaruka, nimetengewa bilioni 1.7, lakini ninachopigana nacho ni kuangalia nani atakwenda kuwekeza pale. Pia imeelezwa kwamba NDC anashindwa kufanya feasibility study, anawategemea wawekezaji. Jambo la muhimu tunalofanya ni kutafuta vijana wazuri wanaoweza kwenda sambamba na wale wawekezaji ili kufanya feasibility study. Si jambo la ajabu, hata kwenye petroleum industry tunafanya hivyo, jambo la muhimu ni kuwa-monitor wanafanya nini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba, ushauri wao ni mzuri na tutauzingatia.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.