Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo; na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) pamoja na Maoni na Mapendekezo yaliyomo katika Taarifa hiyo

MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa nafasi hii lakini vilevile niwashukuru sana Wajumbe wa Kamati ya LAAC pamoja na PAC kwa taarifa yao nzuri ambao kwa kweli wamefanya kwa niaba yetu sisi Bunge zima. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati ya LAAC imekuja na mapendekezo tisa kwa mujibu wa tarifa hii. Mimi naomba nitangulie kusema nayaunga mkono mapendekezo yote hayo ambayo imeyatoa. Kwa kweli ukisoma taarifa hii utaona Kamati hii imechukua muda mwingi sana kufanya kazi. Sisi kama Wabunge kwa sababu kazi hii wamefanya Wabunge wenzetu tunawajibika kuwapongeza sana Wajumbe na uongozi wote wa Kamati hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza lililozungumzwa kwenye Kamati hii na mimi nataka nichangie kidogo kwenye maeneo hayo ni upelekaji wa fedha kwenye Halmashauri zetu. Kila Mbunge aliyesimama hapa amezungumza kwa namna tofauti tofauti namna ambavyo kutokupelekwa kwa fedha za maendeleo kwenye Halmashauri kunavyoathiri miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri zetu. Wewe unafahamu na Bunge linafahamu shughuli nyingi tunazofanya sisi Wabunge zinatekelezwa kwenye ngazi ya Halmashauri, kama Halmashauri hizi hazipatiwi pesa bila shaka mwisho wa siku hatutakuwa na jambo la maana la kujivunia kwamba tumefanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kwenye Wilaya yetu ya Bukombe tumepeleka maombi mbalimbali ya fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Barabara nyingi zilizopo kule kwa muda mrefu hazipitiki kwa sababu maeneo mengi ya Wilaya yetu ya Bukombe yapo kwenye milima, barabara zile zimekatika, hazipitiki. Barabara kama za Maghorofani, Mchangani, Imalanguzu, Nifa, Rulembela na Kelezia hizi zote hazipitiki kwa sababu hazijawahi kufanyiwa matengenezo mwaka uliopita na mwaka huu vilevile hatujawahi kupata fedha. Kwa hiyo, naunga mkono mapendekezo ya Kamati ya kwamba sasa Serikali iharakishe kuzipeleka pesa kwenye Halmashauri ili tuweze kupata maendeleo haya na ukarabati wa miradi hii uweze kukamilika.
kufurahi. Wilaya ya Bukombe na Wilaya nyingine kwenye Mkoa wa Geita na hili nimeliuliza humu Bungeni, nimekwenda TAMISEMI nimewauliza fedha za walimu waliosimamia mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ziko wapi? Wengine wakaniambia uende kwa watu wa Wizara ya Elimu, wengine wanasema hapana nenda TAMISEMI, shilingi milioni 35 walimu wa Bukombe kila tukikutana ndiyo jambo wanaloniuliza. Kila tukionana wananiambia Mheshimiwa pamoja na maneno mazuri uliyonayo kahela ketu kako wapi? Naomba hapa kahela haka kapatikane, watu hawa wapewe chao, watu hawa wajijue na kahela kao haka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesimamisha kupandisha vyeo vya walimu kwa sababu tulikuwa tunashughulikia watumishi hewa, tumesimamisha mishahara iliyokuwa imepandishwa ikarudi ili tumalize jambo la watumishi hewa, hata haka ka kusimamia mitihani na kenyewe kanasimama, hapana! Naomba sana walimu hawa walipwe fedha zao ili waweze kufanya kazi yao kwa juhudi wakiwa wanajua kwamba Serikali inawapenda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ajira ya mwaka jana iliandikwa barua TAMISEMI kwenda kwenye Halmashauri zote walimu wapya walioajiriwa fedha zao zile Halmashauri zichukue kwenye akaunti yoyote pesa zilipe nauli. Wilaya ya Bukombe shilingi milioni 58 zilichukuliwa ni fedha za wakandarasi zikalipa nauli walimu wapya waliokuwa wameajiriwa, zikalipa subsistence allowance kwa ajili ya walimu wale wapya, fedha hizo hazijalipwa, wakandarasi wanatafuta hela, Halmashauri inahaha ipate wapi pesa ya kuweza kuwalipa wakandarasi hawa. Halmashauri hii ikishtakiwa na ambavyo hatuna fedha imani yangu ni kwamba hatuwezi kutoboa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba TAMISEMI kwa barua ile mliyoandika ya kwamba wachukue fedha kwenye akaunti yoyote mtarudisha, rudisheni hizi fedha sasa hivi Halmashauri kule hali ni mbaya. DT hata kukaa kwenye kiti anaona shida, Mkurugenzi kukaa kwenye kiti anaona shida kwa sababu wakandarasi hajui watakuja kwa wakati gani. Naomba Wizara ya TAMISEMI tuhakikishe kwamba madai haya tunayashughulikia haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lipo lililosemwa hapa na watu kwenye Waraka tmezungumzia asilimia kumi ya vijana na akina mama, naomba hili jambo tuanze…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.