Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niweke msimamo kwamba na mimi pamoja na Kambi yetu Rasmi tunakubaliana kimsingi kwamba mkataba huu kwa muda huu usisainiwe na Serikali.
Mheshimiwa Spika, lakini hilo lisitunyime nafasi ya kuweza ku-criticize mkataba mzima objectively. Maprofesa watatu walikuja Jumamosi, ninawaheshimu sana. Mheshimiwa Profesa Kabudi, ni mwanasheria nguli, ni mwalimu wetu kwa namna yoyote, lakini walipowasilisha upande mmoja wa shilingi, kisomi haikubaliki.
Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye article 101 pale inaposomeka; “resources mobilization.” Nataka tu niwaoneshe faida ya mkataba huu pamoja na madhaifu yake mengi, lakini kuna faida fulani.
Mheshimwa Spika, nenda kifungu cha pili; “The objective of joint resource mobilisation is to complement, support and promote in the spirit of interdependence, the efforts of the East African Community Partner States in pursuing alternative sources of funding to support regional integration and the development strategies, in particular the EPA Development Matrix.” Hiyo matrix hatujaletewa.
Mheshimiwa Spika, Maprofesa wangetuonyesha Waheshimiwa Wabunge hiyo development matrix ni kitu gani? Tunapoungana na EU tunakuwa na nafasi kubwa ya ku-negotiate for funding kwa ajili ya miradi ya maendeleo; mkataba huu unasema hivyo. Mkataba huu kwa kiwango chochote una madhaifu makubwa lakini sisi kama nchi tusifikie mahali tukawa ni watu wa kukataa siku zote.
Mheshimiwa Spika, alipoanza Profesa siku ile, alisema kitu kimoja kwamba nchi ya Tanzania na Afrika ya Mashariki kwa ujumla, itapoteza revenue.
Waheshimiwa Wabunge, naomba niwakumbushe kitu kimoja, mwaka 2004 tuliingia mkataba wetu na Kenya na Uganda; East African Customs Union Protocol. Tuliwaachia nchi ya Kenya kwa miaka mitano walipe kodi.
Mheshimiwa Spika, mkataba huo uliisha mwaka 2009. Mwaka 2009 Kenya ikaanza kuingiza bidhaa zake bila kulipa kodi Tanzania, baada ya Tanzania na Uganda kuruhusiwa kuingiza Kenya bidhaa zao wanazotengeneza kwa miaka mitano bila kodi yoyote.
Mheshimiwa Spika, tujiulize kama nchi, hivi baada ya ule mkataba mwaka 2009, viwanda vingapi Mheshimiwa Mwijage tumeanzisha kuanzia siku hiyo? Tumepeleka nini Kenya? Leo hii mnatutuhumu wengine, tumepeleka kabichi, nyanya na vitunguu lakini hatujaanzisha viwanda vya aina yoyote.
Mheshimiwa Spika, wengine mnasema tunautetea mkataba huu kwa sababu tuna maslahi binafsi na nchi za Ulaya, wala siamini hata kidogo. Mimi ni mzalendo na ninaamini ni mzalendo, lakini hivi mfano Tanzania, Waziri wa Fedha anajua, kati ya mataifa matano makubwa yanayochangia Tanzania bajeti yake, ni nchi zipi? Kama kati ya tano hizo, Ulaya zipo nchi tatu.
Mheshimiwa Spika, nafikiri wakati tunakataa mkataba huu, tujiulize maswali ya msingi, moja, hivi ni viwanda gani hivyo ambavyo tunavitetea kwamba tukiingia kwenye mkataba huu tunapoteza bidhaa?
Pili, kwa muda gani nchi yetu ya Tanzania itaweza kujenga viwanda vyake peke yake na kuweza kushindana na masoko haya mengine ya East Africa na Ulaya pia, itatuchukuwa muda gani kujenga viwanda kwa sababu viwanda vingi vipo mfukoni.
Tatu, kama hatutaanzisha viwanda kama nchi, hivi hamuoni kwamba Ulaya wakiingiza bidhaa zao kwenye uchumi kuna kitu kinachoitwa basket of goods, kwa sababu vitaingia kwa bei rahisi mwananchi wa kawaida atakuwa na uwezo wa kuvinunua kwa wingi zaidi.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi tunapata kutoka China tunavitoza kodi ambavyo ni vya hali ya chini kweli, lakini wote tunafahamu, leo ukiletewa bidhaa kutoka Ulaya na China, wote ambao mmesafiri humu duniani, mtakubaliana na mimi kwamba bidhaa ya China na Ulaya vinatofauti kubwa, quality wise, I will go for European goods for sure!
Mheshimiwa Spika, nne, naomba pia nishauri badala ya kukutaa mkataba huu, Bunge tumshauri Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Rais kwenye kikao cha mwisho cha Marais wa Nchi za Afrika Mashariki -Summit ya juzi Arusha au Kenya kikao kimoja cha mwisho, ndiye aliyewaomba wenzake kwamba jamani mkataba huu sisi hatujapitia, ninaomba niunde Technical Committee ambayo itapitia mkataba huu itushauri kama nchi.
Mheshimiwa Spika, Technical Committee ndiyo ile nafikiri ambao wamewasilisha upande mmoja wa shilingi nafikiri siyo vema sana tukawa ni nchi ya kususa na kukataa wakati hatuchukuii hatua madhubuti ya kuweza kubadilisha nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, nishauri kitu kimoja…
TAARIFA...
MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Spika, naomba nipokee taarifa hiyo kwa nia njema kwamba anajaribu kuniambia kwamba ni kweli Mheshimiwa Rais alivyoomba kwamba iiundwe Technical Committee ya kuishauri Serikali imeundwa, lakini bado haijawasilisha mapendekezo yake.
Mheshimiwa Spika, hilo halitunyimi fursa kama Bunge kuiomba Serikali, mkataba huu kwa sasa usitishwe lakini tusikatae moja kwa moja. Uende ukapitiwe tena tuangalie kama negotiating team ya Tanzania inaweza ikabadilisha baadhi ya mambo ambayo tunayataka na bidhaa ambazo tunataka kuzitetea kwa muda na baadaye urudishwe Bungeni.
Mheshimiwa Spika, pili, ninaomba Serikali yetu badala ya kupiga kelele ya kusema tunaandaa viwanda, sasa ifikirie ni muda sahihi wa kuwekeza kwenye viwanda. Hili jambo la kukimbia na kuwa na protection policy kila saa hautatufikisha mahali. Waingereza wanasema, you better run the hard way kwa sababu the easy way you do not go it, kwa sabubu ninyi hamuwezi hata kidogo. Tukiwaachia hata miaka 100 humuwezi kuanzisha viwanda vya kushindana na Ulaya. Ni changamoto kama nchi kwamba, ni lazima kwa muda huu tuamue wote kama jamii tuungane tuwaambie Mawaziri hawa wenye viwanda mifukoni, walete viwanda ili tusiwe wapiga kelele kwenye soko la Afrika Mashariki.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, leo Arusha ukienda kwenye maduka yote vifaa vya Kenya vimejaa, ukiuliza tunapeleka nini Kenya? Utaambiwa maembe na machungwa ya Tanga na unga wa Azam.
Mheshimwa Spika, baada ya kusema hayo, ninaomba mkataba huu usisainiwe, lakini kama nchi tuangalie faida ambazo tunaweza tukazipata kutokana na mkataba huu, badala ya kuanza kulialia na kupiga kelele kwamba sisi hatuwezi, hatuwezi siku zote! Muda unatosha ni muda sasa wa kushindana na Mataifa mengine kama nchi.
Mheshimiwa Spika, tumeingia kwenye AGOA, mmesikia jana Mheshimiwa Mwakyembe amesema tumeuza asilimia nne soko la Marekani, wakati Kenya wameuza 98% they are taking advantage of their industrial power na Tanzania tunabaki kulalamika ni nchi ya kulalamika tu Kiongozi analalamika, wananchi wanalalamika, kama alivyosema Mheshimiwa Lowassa wakati fulani.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana.