Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nami nachukua nafasi hii kukushukuru, lakini vilevile lazima kwanza tukubali. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa namna alivyouona na namna alivyoshaurika. Namshukuru Mheshimiwa Mkapa, Mheshimiwa Msigwa kasema tusikatae kwa sababu tu kuna watu wamesema tuukatae. Tunaukataa kwa sababu mkataba huu ni non starter kwa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, if you don‟t deal with the problem, the problem will deal with you. Hili ni tatizo kubwa sana. Sasa kuna mjumbe amesema tunaukataa kwa sababu kuna watu, viongozi wetu wamesema. Ni kweli viongozi wamesema na wamesema sahihi. Sasa hapa kuna kiongozi kwenye Bunge EU kuna kamati mbili; International Trade na International Development. Hizi kamati nazo hazielewani kuhusu mkataba huu. International Trade wanaushikilia mkataba huu na International Development hawautaki mkataba huu.
Mheshimiwa Spika, sasa kuna mtu kasema tunawasikiliza watu, tumsikilize Mbunge wa European Union anachokisema kuhusu mkataba huu. Anasema: “the agreement to pose a risk to regional economies as their infant industries will face unfair competition due to products from the European Union.
Mheshimiwa Spika, huyu ni Mbunge wa European Union, siyo Mtanzania wala hatoki East Africa. Anasema, she point it out that the European Union had pushed a hard bargain in the deal large by arm twisting Kenya.” Wamewafuata Kenya wakawapinda mkono. Anaendelea kusema, “I think this kind of agreement is unfair for the East African Region; Europe is pushing very hard stance and they have taken Kenya as a leader. Kenya is the only one that has interest in this trade agreement, because they are not a list development country.” Kenya ni non list development country. Siyo list kama sisi.
Mheshimiwa Spika, anasema, Kenya need this agreement to maintain acces to the European Union. Anaendelea kusema; “if the agreement goes through, you East Africans;” anatuambia sisi, hawaambii Kenya, anatuambia wote block, “have no more preferences; you will receive all products coming from Europe in your market which will promote unfair competition.
Mheshimiwa Spika, European competence is high, ni kweli! Hivi maziwa ya salsa yatakuja hapa, wanakuta maziwa yametoka Ulaya ya dola moja badala ya haya ya kwetu ya dola moja na nusu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hili jambo wenyewe wanatutahadharisha. Wanaendelea kusema, so far they have been able to guarantee Kenya access to the EU market without even this agreement.
Mheshimiwa Spika, umeona tunapopelekwa? Kenya kusaini huu mkataba au wasiusaini, tayari wana soko EU. Kwa hiyo, they don‟t need this agreement. We have guarantee Kenya! Hao ni EU wanasema, that we still have access to the European market and to help their market in internal African Market.
Mheshimiwa Spika, mengi tutayasema, nchi hii tukiingia kwenye mkataba huu, tumeua industries ambazo sasa hivi Serikali inataka kujenga.
Mheshimiwa Spika, wewe ni mmoja wa watu ambao wameijengea heshima kubwa sana nchi hii. Kwenye mikutano ya EUSP - Brussels, ndio ulikuwa unasimama na kutuongoza sisi kupinga kitu hiki cha kutuingiza katika matatizo makubwa sana. It goes without saying. Tukisaini mkataba huu, we are done.
Mheshimiwa Spika, illegal fishing inayofanywa kwenye bahari zetu. Tuna-lose 250 million Euros kwa kila mwaka kwa samaki kupelekwa Soko la Ulaya. Samaki hawa wanaibiwa katika bahari zetu, samaki hawa wakifika kwenye Soko la Ulaya wanatozwa kodi kule; na kodi hiyo inabadiki kutumika kwa wananchi wa European Union, sisi hatupati chochote. Nilitegemea kwanza angesema wange-deal na samaki zinazoibiwa kwetu kabla hazijapelekwa kwao kutumia kwa watu wao.
Mheshimiwa Spika, mkataba huu unasema, kukiwa na loses za revenue wataweka mfuko. Hebu tujiulize Waheshimiwa Wabunge, zipo nchi zimeshasaini mkataba huu; Caribbean countries; Mauritius hapa Afrika na kuna nchi za Afrika Magharibi zimeshaanza ku-lose revenues.
Mheshimiwa Spika, masuala ya industries katika nchi zao zimeshaanza kupotea. Mfuko huo walisema unaanzishwa, haujaanzishwa, haupo kwenye bajeti na hakuna popote katika nchi hizi zinazosaidiwa. Sisi wa tatusaidia lini?
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mkataba ni mzuri sana, kwa lugha nzuri iliyoandikwa kisheria, lakini it is a non starter kwa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba Waheshimiwa Wabunge, nchi hii tusimame pamoja kwenye suala hili; one Nation under one God, tusikubali kusaini mkataba huu. Kama kuna nchi imesaini, wana interest zao.
Mheshimiwa Spika, kuna nchi nyingine hawana interest za Kitaifa, wana interest zao binafsi. Tunajua nchi zilizoingia kwenye mikataba hii wanafanya biashara individually, lakini tuulize, soko la maua pesa ngapi zinarudi Kenya na pesa ngapi zinabaki huko zinapopelekwa? Hatutaki kuingia kwenye matatizo kama ya Kenya.
Mheshimiwa Spika, yote haya tunavyosema hapa kwamba Kenya inatumika as a front as a leader ni kuhusu malighafi ambayo Tanzania inayo, nothing else. Na wewe uliwaambia Brussels mkitaka madini yetu, jengeni viwanda kwetu. Tatizo liko wapi? Badala ya kusafirisha madini kutoka hapa kuyapeleka Ulaya, walete viwanda hapa, tuta-promote jobs, tutaweza kupata revenues za kutosha na kusaidia nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, sina haja ya kusema mengi, hili suala linafahamika, na yule anayepinga hili, analipinga tu kuonesha kwamba anasimama, anapinga. Hawana hoja ya msingi.
Mheshimiwa Spika, naunga mjono hoja, tusisaini mkataba huu.