Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuchangia juu ya mkataba huu wa EPA.
Mheshimiwa Spika kwanza nieleze msimamo wangu. Msimamo wangu mimi binafsi, serikali isiusaini huu mkataba. Ninazo sababu za msingi za kusema lakini pia nina maangalizo mengi kwa Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wakati tunahitaji kusaini mkataba huu au tunautazama mkataba huu, kuna haja ya kuangalia Mkataba wa Cotonou (Cotonou Agreement) ambao tulisaini.
Mheshimiwa Spika, ukisoma faida ambazo nchi za Afrika tumezipata kwa kusaini Mkataba wa Cotonou, unaona kwamba tulipata faida moja wapo kubwa ilikuwa ni kwamba tuliweza kuingiza bidhaa zetu katika soko la Ulaya na tukaweza kuokoa zaidi ya Euro billion 1.4 ambayo ilikuwa ni duty and tariff ambayo kama si mkataba ule hizi pesa maana yake tulitakiwa tuzilipe.
Mheshimiwa Spika, tunaposema EPA kwetu sisi haitufai kwa sasa ni kwa sababu moja kubwa. Wenzetu wameweka kifungu cha import duty kuwa free, tujiulize kwetu sisi kama Taifa tuna bidhaa ambazi zinakidhi viwango kuingia kwenye soko la Ulaya? Hili ni swali la msingi sana na je, wenzetu wa Ulaya wanazo bidhaa ambazo zinaweza kuingia zikakidhi vigezo katika soko letu la Tanzania? Hili ni swali la msingi sana la kujiuliza.
Mheshimiwa Spika, lakini pia tujiulize, ikiwa tutaondoa ushuru kwa bidhaa zinazoingia, tutapoteza mapato ya kiwango gani katika bandari yetu ambapo tunategemea import kwa kiwango kikubwa kutoka kwenye hayo mataifa ambayo leo tunaingia nayo mkataba. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo la msingi kuangalia; tunawalaumu wenzetu Kenya kwamba wameharakia, Kenya wenzetu wameandaa facilities na wana bidhaa za kwenda kuuza Ulaya, tayari wanazo. Suala sio kuwalaumu, suala tunatakiwa na sisi tujiandae ili tuweze kuwa na bidhaa zitakazofikia viwango vya kuviuza Ulaya. Kwa hiyo, angalizo ninalolitoa mimi, si tu tunawalaumu Kenya, ni kweli, hatuwezi ku–compete na wenzetu lakini tujione kwamba tumechelewa kwasababu ya uzembe wetu sisi wenyewe. Tumeshindwa kujipanga.
Leo tunakuja kuwalalamikia wenzetu, tuwaache wenzetu waende lakini sisi kama Taifa nasema kwa maslahi mapana ya Taifa hili hatuwezi leo kuusaini kwasababu hatuwezi kushindana nao. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Tanzania tuna sifa ya kusaini mikataba mingi. Ukisoma mikataba, Lome Convention, Cotonou convention - tulisaini lakini maeneo mengi ya vifungu ambavyo tulikubaliana navyo vingi tukashindwa kuvitekeleza, na kimoja wapo cha kifungu ambacho tulisaini kwenye Cotonou Convention ilikuwa ni suala la impunity pamoja na rule of law ambavyo hivi vyote vilikuwepo kwenye Cotonou Agreement, tulishindwa kama Taifa kuvitekeleza, sisi wenyewe.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wakati mwingine tunaposaini mikataba sisi wenyewe tunakuwa hatujajitengenezea mazingira ya kuweza kuendana na mkataba husika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mimi kwa niaba yangu na nashukuru sana kwamba hata chama changu, Chama cha Wananchi CUF kimetuagiza kwamba huu mkataba tuukatae. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, chama chetu kimefanya analysis ya kutosha, na mara nyingi chama chetu kimekuwa na watu makini na tukifanya misimamo mizuri. Mkataba huu, msimamo wa chama chetu tunaukataa.
Kwa hiyo tunaomba Serikali, Mkataba wa Cotonou usiusaini kwa sababu tumechelewa, wenzetu wametuacha sana. Jukumu pekee ambalo tunapaswa kulifanya ni sisi kujipanga kwa sababu wenzetu duniani wanakimbia, tusiendelee kutambaa, ndilo suala la msingi la kulifanya.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Ibara ya 63 ya Katiba yetu, kazi tunayofanya hapa ni kazi ya Kikatiba. Naomba nimalizie kwa kutoa wito, ipo mikataba pia ambayo kama Taifa tumesaini ambayo yenyewe ina mpact kubwa kwenye nchi yetu ikiwemo na Mikataba ya Gesi na Madini.
Mheshimiwa Spika, tengeneza jina, tunaomba mikataba hiyo ya gesi tuilete ndani ya Bunge na yenyewe tuje kuijadili kwa sababu inakwenda kugusa maslahi mapana ya Taifa letu. Nakushukuru kwa kunipa fursa hii.