Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, na mimi nianze kwa kuunga mkono hoja ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuchangia naomba kwanza niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote, kwa kutoa michango yao kwenye mambo mbalimbali yanayohusu uboreshaji wa huduma za afya nchini. Niwahakikishie tumesikiliza kwa makini na tutayafanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda kutoa mchango wangu kama ifuatavyo; kwamba wakati tunaomba kura mwaka jana sisi wa Chama cha Mapinduzi tulizungumzia sana kuleta mabadiliko ya kweli kwenye nchi yetu, na tulipoweka mkakati huu wa kuzungumzia kuleta mabadiliko ya kweli, siyo tu mabadiliko kama waliyozungumzia wenzetu, tulijua wazi kwamba mabadiliko yanakuja na maumivu, na tulijua wazi kwamba mabadiliko yatakuja tu kama kutakuwa kuna uwajibikaji na watu watafanya kazi ipasavyo. Pia tunatambua kuwa mabadiliko ni lazima yatokee, kwa sababu kama kuna kitu kina uhakika wa kubadilika basi ni mabadiliko yenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani, Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli, amepata heshima kubwa sana kwenye duru za Kimataifa kwa kuimarisha mifumo ya uwajibikaji kwenye nchi yetu, lakini pia kwa kurejesha nidhamu ya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwongozo anaoutoa Mheshimiwa Rais, umetuwezesha sisi wa Wizara ya Afya kuboresha huduma kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba utafiti wa TWAWEZA ambao uliwasilishwa takribani miezi miwili iliyopita umeonesha kwamba sekta ya afya inatoa huduma bora, na hii ni kwa mujibu wa utafiti wa sauti za wananchi ambapo wananchi wametoa feedback hiyo, kwamba huduma za afya zimeboreka kwa sababu ya uwajibikaji wa Serikali ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo napenda kuchangia ni kuhusu nia njema ya Serikali kwenye eneo la kuongeza upatikanaji wa dawa nchini. Nia hii inajionyesha wazi kwa Serikali kutenga bajeti ya shilingi bilioni 251.5 ambayo imeanza kutekelezwa mwezi julai mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii shilingi bilioni 70 ndani yake zitakwenda moja kwa moja kununua dawa kwa ajili ya kupeleka kwa wananchi, na mpaka sasa Wizara ya Afya imekwisha pokea shilingi bilioni 20 kwa ajili ya kununua kuanza kupeleka…
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la dawa Serikali pia inaimarisha upatikanaji wa dawa za chemotherapy yaani dawa ya huduma za kansa kwa tiba ya kemikali ambapo mwaka huu tuna shilingi bilioni saba ukilinganisha na shilingi bilioni moja iliyekuwepo mwaka jana. Kwahiyo naomba Waheshimiwa Wabunge watuamini tuna nia njema ya kuboresha huduma za afya nchini, na kufikia mwezi wa 12 tunaahidi tutakuwa tumewezesha upatikanaji wa dawa wa asilimia 85 ukilinganisha na asilimia 63 tuliyonayo kwa sasa.