Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru, na mimi nipitie mapendekezo ya Mpango na zaidi nitoe ufafanuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ambalo nataka kufafanua nilieleze Bunge lako Tukufu na niwaambie Watanzania. Jukumu la ujenzi wa viwanda ni jukumu la sekta binafsi. Soma mpango wa pili wa miaka mitano, soma vision 2020–2025, sikiliza hotuba za Mheshimiwa Rais, ujenzi wa uchumi wa viwanda, kule kujenga viwanda ni jukumu la sekta binafsi. Serikali kazi yetu ni kutengeneza mazingira wezeshi, tutatengeneza miundombinu, tutatengeneza maji, tutapeleka umeme, sekta binafsi ndio itajenga viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ilibidi nilizungumze hili. Sekta binafsi ni nani? Ni mimi Mbunge, mwananchi, mfanyabiashara. Niwaeleze ndugu zangu Wabunge muelewe viwanda maana yake ni nini? Mheshimiwa Waziri Mkuu atawasomea hotuba ya taarifa yangu ya Viwanda vilivyojengwa, wengine mtashangaa na wengine mtapatwa kihoro, kazi imefanyika. Kwa tafsiri ya viwanda ya Benki ya Dunia, kuna kiwanda kinaajiri mtu mmoja mpaka watu wanne kinagharimu shilingi milioni nane, kuna kiwanda kinaajiri watu watano mpaka 49 ni cha shilingi milioni tano mpaka 200, hizo ndizo ambazo nasema zinapatikana na benki zipo tayari kutoa pesa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna viwanda vinaajiri watu 50 mpaka 99 vinathamani ya shilingi milioni 200 mpaka milioni 800 hivyo viwanda vinaitwa viwanda vya kati. Nitumie fursa hii kuwaambia Wabunge wote mnaotoka maeneo ya SAGCOT ziko pesa dola milioni 70 za Kimarekani, anayetaka kwenda kujenga kiwanda aje aniambie nipo Dodoma siku tatu hizi nikamuonyeshe namna ya kuomba. Waambieni watu wenu pesa zipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo tulilolipata katika ujenzi wa viwanda kulingana na taarifa za wataalamu, kama alivyosema ndugu yangu Ulega ni mindset, watu wanalala wanasubiri Serikali ije iwajengee viwanda.
Kwa hiyo hivyo ndivyo vitakavyojengwa na kazi inaonekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze suala la Kurasini Logistic Center. Kurasini Logistic Center Serikali imeshalipa fidia kilichobaki tutamleta operator, ambapo viwanda vita-assemble bidhaa pale zinazotoka nje kuja hapa, lakini pia na kukusanya bidhaa kutoka kwa wananchi kuzi-assemble kwenda nje kuuzwa, ndio utaratibu huo. Masharti anayopewa operator lazima aajiri vijana wa kitanzania ili wapate ujuzi wanaporudi kwao wajue namna ya kutengeneza viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze suala la TBS. TBS inasimamia viwango na nimewaeleza hata Mawaziri wenzangu hata rafiki zangu sitaandika memo kwa mtendaji yeyote wa TBS eti ampendelee mtu yeyote, you follow the principles unapata huduma, wanaolalamika wana makando kando yao, sitaandika memo yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiongozi wa wafanyabiashara bwana Minja amenifuata kwa matatizo ya TBS, niwaambia wataalam wangu wawashughulikie wale wafanyabiashara wadogo watashughulikiwa. Lakini ngoja niwaambie mkilegeza TBS utendaji wake viwanda vyangu vitakufa, ni kama nilivyowaambia jana lazima TBS izuie bidhaa dhaifu na isiyolipa kodi isiingie nchini. Vijana wa TBS wanafanya kazi nzuri na nitaendelea kuwaongezea nguvu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mchuchuma na Liganga. Mchuchuma na Liganga Serikali hakuna tatizo wala hamtaweka pesa zenu kwenye bajeti, muwekezaji yupo ameshapatikana, nimeelekezwa na mamlaka kwamba niandike cabinet paper niipeleke hatua zilizobaki ziweze kupata baraka ya cabinet paper, ikishindikana zitaletwa kwenye Bunge. Kwa hiyo, msiwe na wasi wasi kamanda Silinde kwamba tumepanga Mchuchuma na Liganga, Logistic Center, haiwahusu, ninyi mmeshatoa baraka tunalishughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie wepesi wa kufanya biashara (the easy of doing business). Tulikuwa watu wa 139, tumekuwa watu wa 132, sijaridhika. Kwa hiyo, anayesema kwamba sisi tuna mahusiano mabaya na wafanyabiashara aje aniambie wafanyabiashara anayewawakilisha ni nani. Ukiwataka wafanyabiashara njoo uniambaie mimi, kila siku ninakuwa nao wanazungumza vizuri ila wanasema ukikaza ukaze kwa wote. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri wa Mipango eti ukaze sawia wote mianya uweze kuibana, kwa hiyo, hatuna matatizo, wafanyabiashara wa kweli ni wenzetu. Lakini Waheshimiwa Wabunge mkubali….


niandike cabinet paper niipeleke hatua zilizobaki ziweze kupata baraka ya cabinet paper, ikishindikana zitaletwa kwenye Bunge. Kwa hiyo, msiwe na wasi wasi kamanda Silinde kwamba tumepanga Mchuchuma na Liganga, Logistic Center, haiwahusu, ninyi mmeshatoa baraka tunalishughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie wepesi wa kufanya biashara (the easy of doing business). Tulikuwa watu wa 139, tumekuwa watu wa 132, sijaridhika. Kwa hiyo, anayesema kwamba sisi tuna mahusiano mabaya na wafanyabiashara aje aniambie wafanyabiashara anayewawakilisha ni nani. Ukiwataka wafanyabiashara njoo uniambaie mimi, kila siku ninakuwa nao wanazungumza vizuri ila wanasema ukikaza ukaze kwa wote. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri wa Mipango eti ukaze sawia wote mianya uweze kuibana, kwa hiyo, hatuna matatizo, wafanyabiashara wa kweli ni wenzetu. Lakini Waheshimiwa Wabunge mkubali….
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwijage naomba umalize.