Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yoyote na mimi nianze kwa kuipongeza Serikali na kuunga mkono hoja hii. Lakini kutokana na ufinyu wa muda naomba nizungumze mambo makubwa matatu halafu nitajielekeza katika ya mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo yenyewe ni kama ifuatavyo, na ningeomba sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wayachukue mambo haya
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kariakoo ni sehemu yetu ya biashara tunayoweza kuiita ni sehemu ya biashara ya kimataifa. Hivi sasa Kariakoo inahudumia zaidi ya nchi tano za Kiafika ikiwa na sisi wenyewe wa ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu tulikuwa na tatizo bandarini, lakini hapa karibuni kwa takribani wiki mbili, tatu, mwezi tatizo la upatikanaji wa mizigo kwa ajili ya soko letu hili la Kariakoo, kwa maana eneo la Kariakoo limejitokeza kutokana na agizo lile la kwako Mheshimiwa Waziri la TBS. Nomba nikueleze kuwa jambo hili siyo baya, lakini nataka hili jambo la TBS uweze kuliweka vizuri na elimu kwa wafanyabiashara wale iende sawasawa.
Mheshimiwa Waziri, wafanyabiashara wa Kariakoo wengine ni wafanyabiashara wadogo wadogo ambao ni wanakusanya mitaji yao wanaunganisha katika kontena moja. Mmoja tu anapokosa kukutana na SGS, wakala wetu shida kubwa inatokea pale bandarini. Nataka nikuambia storage ya wafanyabiashara wale wa Kariakoo hivi sasa imekuwa kubwa sana na mitaji yao inakatika.
Nakuomba sana jambo hili uliingilie uone ni namna gani ya kuweza kuwasaidia ili waweze kuendesha maisha yao na hatimaye biashara iendelee kuweza ku-propel katika eneo hili la biashara la Kariakoo.
Mheshimiwa mwenyekiti, naomba nizungumzie BRT, nimeiona katika Mpango wa Maendeleo wa Mwaka huu wa 2017/2018. Naomba nisisitize ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja Mkuranga, alisema kwamba BRT itakwenda mpaka Mkuranga, itavuka pale maeneo ya Mbagala. Naomba iende kwa sababu tunalo eneo zuri la Serikali, linaweza kutusaidia kwa kazi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jana yuko msemaji mmoja hapa alisema hakuna viwanda vipya. Nikuombe Mheshimiwa Waziri uwachukue baadhi ya Wabunge walete kule Mkuranga wakione kiwanda cha Good Will Ceramics kipya ambacho zaidi ya shilingi bilioni 200 zimewekwa pale na tunategemea zaidi ya wafanyakazi 4,500; watu wa Mtwara, Lindi wanajua kiwanda kile cha kilometa moja kinachojengwa pale Mkuranga, naomba jitihada hizo zifanyike zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba pia ulitangaze eneo la Mkiu kuwa ni eneo rasmi la viwanda. Tunazo ekari nyingi pale hazihitaji compensation, walete. Na naomba uwabadilishe mindset Waheshimiwa Wabunge hawa, mambo ya kuwaza kiwanda kikubwa sana kama kile cha Mkiu Mkuranga waachane nayo. Viwanda vidogo vidogo vya dola 5,000, 10,000, ardhi tunayo pale, waje wawekeze katika kubangua korosho. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie na maneno yafuatayo ya ahadi ya Mheshimiwa Rais. Wakati Mheshimiwa Rais anachukua nchi hii mwezi Novemba, 2015 aliahidi kupambana na rushwa, aliahidi kufanya kazi kubwa ya kuzuia matumizi yasiyokuwa mazuri ya pesa za umma pamoja na kushughulika na watu wasiokwepa kodi. Mheshimiwa Rais alipokuja Mkuranga alieleza wazi hana tatizo na wafanyabiashara akitumia uwanja ule wa Bakhresa. Watu leo humu ndani wanazungumza kwamba Serikali hii haina urafiki na wafanyabiashara.
Mheshimiwa Rais aliwaeleza wazi mfanyabiashara anayelipa kodi huyo atakuwa ni rafiki yake, lakini mfanyabiashara asiyelipa kodi hana urafiki naye. Nataka niwaambieni IMF wametoa ripoti Jumatatu, timu ile inaongozwa na mtaalam mmoja anayeitwa Mauricio Villafuerte. Huyu bwana ameeleza wazi, ameeleza namna nzuri ambayo tunakwenda nayo, lakini wametushauri pia juu ya kujaribu kurahisisha kidogo juu ya mzunguko wetu wa fedha na mengineyo, lakini wametupongeza na wamefikia hatua nzuri ya kuwaambia Watanzania kwamba hata madeni ya nje na mengineyo sasa tuko vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nataka nimalizie na maneno ya Mwenyezi Mungu katika kitabu kitakatifu cha Qurani. Mwenyezi Mungu subhana wa ta’ala anasema katika Qurani tukufu kama ifuatavyo; “Na wale wanaojitahidi kwa ajili yetu tutawaongoza njia zetu. Nasema fanyeni kazi basi ataona Mwenyezi Mungu vitendo vyenu na Mtume wake na waumini wataviona vitendo vyenu. Enyi wanangu wala msikate tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu, hawakati tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu waliokosa imani.”
Mheshimiwa Mwenyekiti wale watu waliokosa imani wote wamepotea. Leo mkubwa mmoja amekuja humu ndani anahangaika, anaweweseka, nazungumzia shilingi milioni 10, kama anazitaka zile shilingi milioni 10 aje timu kubwa huku CCM asikate tamaa wamebanwa.
heshimiwa Mwenyekiti, nashukura sana naunga mkono hoja.