Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia katika hoja hii iliyopo hapa mbele yetu. Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri na wataalam wote walioshiriki katika kuandaa mpango huu ili na sisi tupate fursa ya kuuchangia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite kwanza kabisa kwenye viwanda, tunapozungumzia viwanda ni lazima tuwe na viwanda mama na wengi sana wamezungumzia habari ya Mchuchuma na Liganga. Hadithi ya Mchuchuma na Liganga sasa inafikia mahala itabidi hata watoto wetu tuwabatize majina hayo, kwa sababu hadithi hii ni ya miaka mingi sana. Mchuchuma na Liganga lakini ukweli wa mambo ni kwamba wengi tunaongelea Mchuchuma na Liganga tunafikiri Mchuchuma na Liganga viko mahala pamoja. Kutoka Liganga mpaka Mchuchuma kuna umbali wa takribani kilometa 80 au zaidi na Mchuchuma ni mahala ambapo makaa ya mawe yanapatikana. Na Liganga ni mahali ambapo chuma kipo sasa ukiangalia utaona kwamba tumeiweka hii miradi pamoja tukiamini kwamba ni mradi mmoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuona kwamba Serikali sasa ione itenganishe miradi hii, makaa ya mawe yaliyoko mchuchuma yaanze kutoka, kwa sababu utoaji wa makaa ya mawe hauitaji mitambo ya ajabu, hauhitaji vitu vikubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachohitaji katika Mkoa wa Njombe tunahitaji barabara ile itengenezwe, tumeambiwa habari ya barabara miaka ilani ya uchaguzi iliyopita ilisema barabara ya Itoni - Manda, ilani hii kuna Itoni - Manda. Kumetengwa kilometa 50 barabara ina zaidi ya kilometa 150, lakini zimewekwa kilometa 50, hasa unaweza ukaona kwamba ni kiasi gani tuko serious. (Makofi)
Sasa tunahitaji nani muwekezaji aje awekeze kuchimba chuma kwa sababu pale tumekuwa tukisimulia mpaka hadithi za ajabu ajabu, kwamba chumba kile kikianza kuchimbwa malori 600 yatapita kila siku kwenye Mji wa Njombe kusafirisha chuma. Hasa barabara ya vumbi malori 600 hiyo itakuwa ni barabara kweli, hebu tuone are we serious kweli kuhakikisha kwamba kile chuma kinataka kutoka, are we serious kwamba tunataka yale makaa yatoke? Kwa hiyo, niombe sasa Serikali ione itenganishe miradi hii makaa yaanze kutoka kwa sababu makaa hayaitaji utaalamu sana. Lakini vilevile barabara hii ya Itoni - Manda itengenezwe ili kusudi sasa iweze kufanya kazi ya kupeleka maendeleo upande ule na mali zile ziweze kutoka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ambalo ningependa kuliongelea leo ni suala la elimu, nimekuwa nikipitia katika kitabu cha mpango hiki ukurasa wa 53, unaeleza mpango kabambe wa elimu msingi. Ndugu zangu elimu msingi ni kitu kigumu sana kama nchi hii hatujawahi kupata maanguko makubwa tunakwenda kupata maanguko sasa kwenye elimu msingi, kwa sababu elimu msingi inaonyesha kwamba watoto walioko darasa la pili sasa wataishia darasa la sita. Ina maana kwamba mwaka 2011 watoto hawa watakuwa form one, lakini wakati huo huo wale walioko darasa la tatu na wao watakuwa form one.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ina maana shule za sekondari tulizonazo zitakuwa na mikondo miwili, na mkondo mkubwa ni huo wa watoto ambao wataishia darasa la sita kwa sababu hawa darasa zima litakuwa linaenda sekondari. Sasa tujiulize leo hii tuna suasua na shule zetu za kata hazijakamilika, kwanza watoto hawa watakuwa na umri mdogo sana kumtoa darasa la sita kumpeleka form one, je, atamudu masomo ya sekondari na atamudu umbali? Watoto wengine tumewapangishia mtaani, watoto wengine wanatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Tuone sasa kama Serikali tunajipangaje kuhakikisha kwamba hii elimu msingi inatekelezwa, vinginevyo tutaenda kutesa watoto, tutaenda kuharibu elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati huo huo elimu kwa uma haipo, nani anajua leo hii kama mtoto aliepo darasa la pili ataishia darasa la sita na ataanza form one. Niwaombe sana Serikali hebu jaribuni kuona sasa pamoja na kueleza kwamba kuna mpango kabambe toeni elimu kwa umma ili kusudi umma ujue kwamba watoto walioko darasa la pili hawa wataishia darasa la sita na wataanza form one. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nizungumzie suala la sekta binafsi, sekta binafsi ni tamu sana kuitamka katika midomo ya Serikali na wadau mbalimbali. Lakini ukija ukweli wake unakuja kuona kwamba kuna ugumu mkubwa sana wa sekta binafsi inakabiliwa nao. Kwanza kabisa sekta binafsi imekuwa kama yatima, haipati msaada wa aina yoyote zaidi ya maneneo lakini wamezungumzia kwamba bajeti ya kodi. Suala la kodi naomba liangaliwe sana sasa hivi karibu kila mtu anadaiwa…
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ahsante