Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia mapendekezo ya Mpango na Mwongozo wa Bajeti.
Kwanza nianze kumpongeza Waziri na timu yake kwa mapendekezo mazuri sana ambayo yanaelekeza ni namna gani kwa mwaka unaokuja tutatekeleza maendeleo ya nchi yetu. Pia nampongeza kwa jinsi alivyojaribu kuangalia review kwa kipindi kilichopita na kutulinganisha na sisi na nchi zetu ambazo zinatuzunguka tuna-perform namna gani? Nafikiri huo ni muendelezo mzuri kwa sababu katika nchi yoyote katika dunia ya leo ya ushindani, nchi kama ya kwetu lazima tuangalie ni namna gani tunashindana na majirani zetu, ni namna gani tunashindana vilevile na mashirika mengine ambayo yanatuzunguka. Kwa hiyo, hilo nakupongeza sana Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo nina mapendekezo machache la mapato, unapoongelea matumizi ni lazima kuwe na mapato ya uhakika. Nchi yetu imejaaliwa neema kubwa mno, naona mapendekezo kwa kiasi kikubwa yanajilenga mno kwenye mapato ya ndani (tax revenue). Nilikuwa naomba sana Waziri jaribu kuangalia ni namna gani tukuze mapato ya non revenue hasa kutokana na investment tulizoziweka kwenye mashirika yetu. Hali ilivyo sasa haya mashirika yanahitaji msukumo ili yaweze kuzalisha mapato ya kutosha na yaongeze Pato la Taifa ili tuwe na hela nyingi, tuwe na vyanzo vingi ambavyo vina uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mojawapo ambalo linatakiwa lisimamiwe ni lile la kuangalia kwamba mashirika yetu yanatekeleza yale majukumu yake ya msingi na yasifanye vitu ambavyo haviko katika msingi wa shughuli ambazo tulikuwa tunazitegemea. Kwa mifano, mashirika yetu ya pension funds mengi yalienda kujiingiza kwenye kuwekeza kwenye majengo. Shirika letu la National Health (NHIF) nalo kwa kiasi kikubwa badala ya kuangalia kuboresha afya nalo likajiingiza kwenye real estate.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unapoangalia ni namna gani tunaweza ku-finance zahanati, vituo vya afya nafikiri tungeitumia NHIF tusingepata shida sana hapa, tungetimiza lengo letu la kujenga zahanati kwa kila kijiji, vituo vya afya kwa kutumia hela ya NHIF. Kwa sababu Halmashauri zinauwezo wa kulipa hilo deni kutokana na mapato ya hizo zahanati na vituo vya afya. Kwa hiyo, naomba jaribu kuliangalia hilo tutoke kule tulikozoea tuende kwenye njia mpya ambazo zinaweza ku-finance bajeti yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine wenzangu wameliongelea sana suala la kilimo. Viwanda na kilimo vinaenda pamoja, unapoongelea viwanda tuongelee ni namna gani tutaboresha kilimo chetu. Kwa mfano, kwa Jimbo langu la Mbeya Vijijini mkituwezesha kulima pareto na kahawa ili tuweze kushindana na Kenya, Rwanda, Ethiopia tuna uwezo wa kuleta pato kubwa sana kwa nchi hii tena la forex.