Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii jioni hii. Naomba niende moja kwa moja kwenye mchango wangu nikiangalia vipaumbele vilivyoainishwa kwenye huu mpango. Nimesoma vipaumbele vyote vilivyotajwa sijaona kipaumbele cha kilimo na sisi tunajitangaza kwamba tunataka kwenda kwenye Taifa la viwanda. Lakini kwenye miradi hii ambayo imetekelezwa, hakuna mradi hata mmoja wa kilimo uliotajwa hapa. Nikifika na kwenye miradi ambayo inatekelezwa nako vilevile sijapata mradi hata mmoja wa kilimo unaotekelezwa zaidi ya kuona kuna Kijiji cha Kilimo Morogoro. Sasa je, hilo shamba ni la mazao gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, si hivyo tu, ulaji wetu kama Watanzania sasa hivi umebadilika, sasa hivi tunakula sana kwenye mazao ya chakula (ngano) kuliko mazao ya mahindi au mchele kama tulivyozoea. Lakini kwenye mpango huu sijaona mahali popote ilipotajwa kuendeleza hili zao la ngano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na mashamba ya ngano NAFCO, yale mashamba sijui yamepotelea wapi. Na hapa nataka ni-declare interest, mimi ni msindikaji wa nafaka. Ngano hii kiwanda kimoja cha Bakhresa peke yake anasindika tani 2,700 per day na hizi tani 2,700 anazosindika kwa siku zinatoka nje a hundred percent, Tanzania tumelala. Leo hii tunakuja tunasema kwamba tunataka kuimarisha viwanda, hapo napo sijapaelewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nirejee kwenye takwimu, hizi takwimu za Mheshimiwa Mpango bado hazijanishawishi. Kwa sababu kwenye akiba ya fedha, pesa za kigeni, tunasema tunayo akiba ya pesa kuendesha miezi 4.1, hapohapo mwisho kabisa anasema kwamba hii ni zaidi ya lengo la chini kabisa ambalo ni la miezi minne. Huko kuongeza tu kwa pointi moja tayari ni sifa kwetu kuona kwamba tumepiga hatua, lakini je, hizi takwimu zinalingana na takwimu za ongezeko letu Watanzania?
Mheshimiwa Mwenyekiti, maana unaweza kujisifu kwamba wewe ni mtu wa kwanza darasani kwa kupata asilimia 30, ndiyo hiki ninachokiona hapa, lakini kama kweli tuna nia nzuri ya kuwatendea haki Watanzania, naomba kabla hatujafika kwenye mpango huu turejee kwanza kwenye sensa ya watu waetu ili huu mpango na haya maendeleo tunayojisifu kwamba uchumi wetu unaimarika, unalingana na idadi ya watu tulionao unaowahudumia huu mpango? Ndiyo maana leo hii Serikali inasema uchumi umeimarika, lakini kwa watu tunaokaa nao wanaona hakuna kitu kinachofanyika, ni kwa sababu ule uchumi unaowahudumia ni wengi kuliko hivyo mnavyotarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nataka nijielekeze kwenye kufungamanisha maendeleo ya watu na uchumi, hapa napo mmetuacha mbali sana. Leo hii tunaposema hivi, tumeacha vijana wanahangaika, kilimo ambacho kinaajiri watu wengi bado ni kilimo chetu kilimo cha mkono. Zipo taasisi zinakopesha matrekta kwa ajili ya kilimo, lakini hizi taasisi sharti la kwanza uwe na hatimiliki ya shamba. Leo hii nani mkulima wa kijijini anaweza ku-access kupata hatimiliki ya shamba, tunawaacha wapi hawa vijana, na hii tunaposema tunafungamisha maendeleo ya uchumi na watu wetu tumewaacha wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, turejee kwenye sekta binafsi, sekta binafsi sasa hivi ndiyo imechukua ajira kubwa sana, lakini hivi asubuhi hapa nimeuliza swali, ni asilimia ngapi ya Watanzania wana hudumu kwenye hivyo viwanda. Lile swali nimeuliza asubuhi hapa sasa nina messages zaidi ya 100 kwenye simu yangu, watu wanasema kweli wanateseka. Nimepigiwa simu kutoka Arusha, Dar es Salaam, Mbeya, watu wanalalamika, hivi viwanda wanahudumiwa na watu wa nje tu, hakuna Mtanzania anakwenda pale akapata ajira, lakini Watanzania bado tunasema tunahimiza uwekezaji. Lakini je, tunapohimiza uwekezaji tupo tayari kufuatilia hawa wawekezaji kwamba wanakidhi masharti ya nchi yetu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kwa upande wa umiliki wa ardhi. Kumiliki ardhi hapa kwetu tatizo ni kubwa sana na hakuna mtu ambaye anaweza ku-access, mtu wa kijijini akaweza kupata hakimiliki. Upimaji sasa hivi wanasema kwamba eka moja ni shilingi 300,000, kitu kama hicho. Sasa hivi mtu wa kijijini ili aweze kupata shamba la eka 10, 20 atahitaji pesa kiasi gani na atazipata wapi? Kwa hiyo, naona huu mpango, pamoja na kwamba nia ni nzuri, lakini utekelezaji wake na upangaji wake haufanani na hali halisi ya watu wetu wanavyoishi huko vijijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kwa upande wa…
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.