Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuchangia katika hoja ambayo ipo katika Bunge lako Tukufu. Moja kwa moja ningependa kuanza na suala la himaya ya pamoja ya ushuru wa forodha (single customs territory). Hii single customs territoryilianza mwaka 2013 lakini utekelezaji wake katika nchi za Afrika Mashariki ulianza mwaka 2014, Kenya na Uganda walianza Januari lakini ilivyofika Julai Tanzania na Rwanda nazo zikaanza utekelezaji wake hadi hivi ninavyozungumza wenzetu wa Burundi bado hawajaanza kutekeleza hii dhana nzima ya single customs territory.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanini nasema haya? Nayasema haya kwa sababu hili ni eneo mojawapo ambalo sisi kama Tanzania inawezekana ikawa tumepigwa goli kwa sababu hii mizigo ambayo inakwenda Kongo sisi tunapo-charge hapa katika Tanzania halafu wengine hawafanyi hivyo ndio hii sasa ambayo wenzetu wanatumia mwanya kupitisha bandari nyingine hizo ili kukwepa hii single customs territory.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninaomba nitoe ushauri kwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana na Serikali kwa ujumla kwamba kwa kuwa hii single customs territory imeanza kwa nchi za Afrika Mashariki na nchi ya Kongo walivyoona kwamba ina manufaa wakaomba wao wenyewe kwamba bidhaa zinazokwenda katika nchi yao zitozwe kodi katika maeneo yetu. Basi naiomba Serikali sasa iweze kuwaandikia Kongo ikiwezekana pia wawaombe na Mozambique nao waingie katika huu utaratibu ili kwamba bandari zote ziwe fair. Lakini kama sisi tutaendelea kutekeleza wakati Mombasa hawatekelezi kwa asilimia 100 na kule Beira hawamo kabisa katika mpango huu na kule Walvis Bay kule Namibia pia hawamo katika mpango huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili ni jambo la Serikali kwa kuwa limeamuliwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki basi warudi kule wakahakikishe kwamba mambo haya yanatekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo lina faida ambayo faida yenyewe imejificha sana sio rahisi kuonekana kwa jicho la karibu. Faida namba moja ni kwamba kabla ya utaratibu huu haujaanzishwa mizigo mingi ya kwenda Kongo ilikuwa inakuwa dumped katika nchi yetu, mizigo ambayo inatakiwa kwenda transit haiendi inabaki katika soko la ndani, matokeo yake ni kwamba nchi inakosa uwezo wa kukusanya kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hiyo, pia wakati huo hata wasafirishaji waliokuwa wanapeleka mizigo Kongo unaweza ukakuta lori limefika Kongo, akaa zaidi ya mwezi mwenye mzigo hajalipa mwezi mwenye mzigo hajalipa kodi kwa hiyo anashindwa kushusha, unakuta unatumia muda mrefu nina ushahidi wa wazi kabisa mimi ni-declare interest nilikuwa ni mdau katika eneo hili, yapo malori ambayo yanaweza yakafanya trip mbili kwa mwaka huko nyuma, lakini baada ya hii single customs territory kuanza kila mtu anaondoka hapa na mzigo ambao umelipiwa kodi anashusha kwa wakati na anarudi na tumekuwa tunatengeneza mpaka trip nane kwa mwaka. Kwa hiyo, ni jambo zuri lakini lazima lifanyiwe utafiti vizuri tuhakikishe kwamba utekelezaji wake usiwe wa nchi moja bali uwe wa Jumuiya nzima ya Afrika Mashariki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilo pia nizungumzie suala zima la mpango pamoja na dhana nzima ya kilimo, kwamba ni kweli kwamba huoni connection ya moja kwa moja kati ya kilimo na hii dhana nzima ya uanzishwaji wa viwanda. Kwa hiyo, ningependa kuwashauri Serikali kwamba sasa hebu ije na comprehensive information ya kuweza kufanya integration kati ya kilimo kitaungana vipi kwenda kwenye viwanda. Hivi viwanda ambavyo mjomba wangu Mheshimiwa Mwijage anavinadi lazima tupate tafsiri ni viwanda vya namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ninavyofahamu mimi kwa Tanzania yetu kwa sababu sisi ni wakulima basi viwanda hivi vinatakiwa viwe vingi vya maeneo yanayoendana na mazao ya kilimo ili tutengeneze wigo mpana wa kuwasaidia wananchi wetu. Hatutarajii kuwa na kiwanda pekee kitakacho ajiri watu 500 lakini tunataka tuwe na kiwanda ambacho kitaajiri watu 500 kwenye kiwanda wafanye kazi za kiwanda, lakini hawa outgrowers huku nje nao waweze kuwa supported, watu wawe busy kwenye mashamba na wawe na masoko ya uhakika kupitia hivi viwanda ambavyo tunakusudia kuvianzisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika hili ni lazima hata tafiti za kilimo zifanyike upya. Sasa hivi wakulima wetu wengi wanafanya kazi hizi za kilimo kwa mazoea, tunazungumzia tatizo kubwa la mabadiliko ya tabia nchi duniani. Hali ya hewa imebadilika, tunaona hata mvua zinachelewa sio kwa wakati kama ilivyokuwa zamani. Kwa hiyo, hii yote inategemea pia na watu wa tafiti nao waende mbali zaidi watafiti kwa hali ya hewa iliyopo sasa ni mazao gani tuyapande yanayoendana na hali ya hewa husika? Kwa hiyo, niishauri Serikali kwamba eneo hilo ni lazima walifanyie mkazo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo mazao ya biashara, mkonge, kule kwetu Mkoa wa Tanga tunalima sana mkonge na takribani mashamba 56 yaliyopo nchini, mashamba 36 yapo Mkoa wa Tanga. Kwa hiyo, naomba eneo hili pia lipewe kipaumbele ili kuweza kukuza uchumi wa Mkoa wa Tanga na nchi kwa ujumla. Ahsante sana.