Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KANGI A.N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru pia kunipa nafasi ya mwisho katika kuchangia hoja ya Mpango wa Maendeleo ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kabisa kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge wenzangu, sisi ni binadamu husahau, sisi ni binadamu ambao wakati mwingine hatuwezi tukaukubali ukweli hata kama ukweli utabaki kuwa ukweli. Niwakumbushe Wabunge wenzangu kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizindua Bunge hili pamoja na mambo mengine aliliomba Bunge hili, alituomba Wabunge kwamba ameomba kazi ya kutumbua majipu tumsaidie ahakikishe anatumbua majipu katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia aliliomba Bunge hili limsaidie pale anapoleta mipango yake ya Serikali tumsaidie ili mipango hiyo iweze kutekelezeka, tuweze kuijenga nchi yetu. Hata hivyo, Bunge hili sasa linapoteza mwelekeo, limepoteza kumbukumbu limebaki sasa ni Bunge la kumlaumu Rais, limebaki ni Bunge la kulialia. Bunge hili litakuwa halimtendei haki Mheshimiwa Rais wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiwa Rais ana nia njema na Taifa, najua Mheshimiwa Rais kwa kauli mbiu ya hapa kazi tu inasababisha watu ambao walikuwa wanaishi kwa mazoea waweze kumlaumu na kumlilia kwamba anaharibu nchi yao. Tunamtia moyo, tunamwunga mkono aendelee kushika na kukandamiza mahali ambapo amekandamiza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mazoea ni ya ajabu sana, tulizoea kwa makundi, wako wafanyabiashara walizoea kukwepa kodi, leo wameshikwa pabaya wanaanza kulia kwamba sasa biashara imekufa. Watumishi tulizoea posho za hapa na pale, tulizoea kusafiri, sasa wameshikwa pabaya wanaanza kulialia. Wabunge tulizoea kwenye Kamati tunapata chai nzuri, tunakula andazi la inchi kumi na nane leo tunakula andazi la sentimita mbili, tumeshikwa pabaya tunaanza kulialia. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge sasa tunaanza kulialia kwa sababu tumeshikwa pabaya na kuwaingiza wananchi wanyonge kwamba wao ndiyo wanaonewa kwamba wao ndiyo hawana fedha. Mambo mengine ni ya ajabu sana, mpaka unajiuliza huyu ndiye Mheshimiwa Mbowe? Mbowe naye leo anailaumu Serikali imefilisika! Hivi ni Mbowe huyu kweli ambaye analipiwa gari na Serikali, shangingi, mafuta yamejaa, kiyoyozi kiko masaa 24, anasema Serikali imefilisika? Huku ni kuwatumia wananchi vibaya, ni kutaka kuwachonganisha wananchi na Serikali yao na Rais wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Msigwa kwa bahati mbaya leo hayupo, Mheshimiwa Msigwa yeye kama Mchungaji nilitarajia atatumia taaluma yake kuwashauri wenziwe kwamba hata wakati ule kwenye Biblia wakati Musa anawachukua wana wa Israel kutoka Misri awapeleke kwenye nchi ya ahadi, nchi yenye maisha mazuri jangwani walipata shida, hawana maji, wanang’atwa na nyoka lakini hatimaye kwa kuwa walikuwa na Mungu, Musa aliwafikisha salama na wakaishi maisha mazuri. Mheshimiwa Msigwa awashauri wenzake kwamba katika safari hii kutakuwa na misukosuko ya hapa na pale, lakini Musa wetu Mheshimiwa Rais Magufuli anatupeleka nchi ya Kaanani twende kuishi maisha ya asali. (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo pia machache ya kumshauri Rais wetu wa nchi hii. Rais wetu alituahidi kwamba sisi Watanzania ambapo yeye ni dereva na sisi ni abiria wake anatusafirisha kutoka mahali tulipopandia basi atupeleke kwenye nchi ya ahadi. Namshauri Mheshimiwa Rais barabarani yeye kama dereva kuna matuta lazima ajue matuta haya akiendesha vibaya yataleta ajali na Watanzania hatutafika mahali anapotupeleka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshauri pia anapoendesha gari kuna zebra cross, wanafunzi wana-cross, ng’ombe wanapita, aendeshe vizuri Watanzania atufikishe salama. Naomba nimshauri pia anapoona wameandika speed 50 na yeye aende speed 50 ili Watanzania atufikishe salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu Mpango nimeusoma, Mpango huu ni mzuri, yako maeneo ya kushauri. Tunayo dira yetu ya Taifa ya Maendeleo 2025, tunayo Ilani ya CCM, vitabu hivi viwili ndivyo vinavyomsaidia Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango katika kuja na mapendekezo mazuri ambayo yanaenda sambamba na utekelezaji wa Ilani ya CCM. Mheshimiwa Waziri yako maeneo humu ambayo inabidi nimshauri, kwenye Ilani yetu kuna mambo ya kilimo, kwenye mambo ya kilimo mpango wake umeacha kabisa mazao ya biashara kama vile pamba, tumbaku, kahawa, katani na pamba pamoja na mazao mengine imeshuka sana. Nimpe mfano, mwaka 2012/2013, tulizalisha pamba tani 356,000 na 2016/2017 imeshuka mpaka tani 120,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni nini? Kama leo watoto wetu wa maskini wanakosa mikopo ya elimu ya juu…
Kimbilio lao ni kwa wazazi wao ambao wanalima pamba. Kama wazazi wao wanalima pamba na humu hajaweka mpango wa kusaidia zao la biashara la pamba, watoto wa maskini hawatasoma, watoto hawa watakuwa wa mitaani. Namshauri atakapoleta Februari rasimu yake isheheni masuala ya kilimo cha mazao ya biashara, masuala ya mbolea ili watoto wa maskini waweze kupata elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani Mheshimiwa Waziri ameweka kanda maalum za kiuchumi. Kanda maalum za kiuchumi Mheshimiwa Mpango tuna Ziwa Viktoria katika nchi yetu, zawadi ambayo tumepewa na Mwenyezi Mungu. Hata hivyo, maji ya Ziwa Viktoria yamebaki kunufaisha Sudan na Misri wakati sisi wa Mikoa ya Kagera, Geita, Tabora, Shinyanga, Mara na Mwanza tunatakiwa tuwe na miradi mikubwa ya uzalishaji kwa sababu tuna maji na ardhi nzuri. Kwa hiyo, Ziwa Viktoria liwekwe kwenye kanda maalum za kiuchumi ili tuweze kuzalisha kwa wingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni eneo la elimu ya juu. Kwenye Ilani tulisema tutajenga Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere, Wilaya ya Butiama. Sasa kama mpaka leo Waziri analeta mpango hauoneshi kwamba tutajenga Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere Butiama na ujenzi wa chuo kikuu ni miundombinu mikubwa, chuo hicho kitajengwa lini Mheshimiwa Mpango? Namwomba kwenye rasimu yake aje na mpango wa kujenga Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere pale Butiama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mwana CCM ambaye niliapa kabisa nitasema kweli daima. Ninyi Mawaziri wa Serikali yangu ya CCM na ninyi ni abiria kwenye basi analoendesha Rais wetu na ninyi mmekaa siti za mbele, wakati mwingine abiria ndiyo humchochea dereva kwamba mnataka kufika mapema. Baadhi ya Mawaziri msimdanganye Rais, msimpotoshe Rais…
Asije akatuletea matatizo kwa sababu Rais anatakiwa ashauriwe vizuri, Rais wetu siyo mchumi. Hivi kweli mtamshaurije Rais kwamba kupotea kwa pesa ni kwa sababu watu wameficha kwenye magodoro, haiwezekani!
Pesa zimepotea kwa sababu Benki Kuu wamezichukua kutoka kwenye mabenki maana yake hazionekani. Pesa zimepotea, mshaurini ni kwa sababu madeni ya ndani hayalipwi, mumshauri vizuri. Itakuwaje mnamshauri Rais kununua ndege kwa cash wakati…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.