Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni lini Serikali kwanza, itamteua Kamishna wa Dawa za Kulevya ili kuleta ufanisi wa kazi katika Tume, maana ni muda mrefu tangu aliyekuwa Kamishna muda wake kwisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwa nini Serikali mmeamua kupeleka fedha za methadon (MDH), badala ya kupitia kwenye Tume ya Dawa za Kulevya kama ilivyokuwa zamani? Serikali haioni kuwa fedha hizo zitakuwa hazifiki kwa wakati kwenye vituo husika vinavyotoa huduma hiyo ya methadon kwa vijana walioathirika na dawa za kulevya?
Tatu, kumekuwa na mkakati wa kuvuruga utaratibu mzima wa kuwarudisha vijana walioathirika na dawa za kulevya kurudi kwenye hali yao ya kawaida, ambapo wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya huenda kwenye vituo vinavyotoa huduma ya methadon kwa kuwashawishi vijana kuanza kutumia tena dawa za kulevya. Kitendo hicho kinarudisha nyuma jitihada za kupambana na dawa za kulevya. Je, Serikali mna mkakati gani wa kuhakikisha mkakati huo unakwama?