Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye Mpango huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naendeleza pale alipoishia Mheshimiwa Bashe, Waheshimiwa Wabunge wa CCM tusipokuwa wakweli hii ni Serikali yetu, ni Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tusipomwambia ukweli Waziri wa Fedha tunakwenda kugonga mwamba. Leo tunapoongelea uchumi kuna tatizo la mzunguko wa fedha ndani ya nchi yetu, unajiuliza fedha zimekwenda wapi? Halafu unakuja hapa unasema uchumi mzuri, sijui nini, how! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mabenki yanaanza kufilisika, Twiga tayari imeshakuwa taken over, CRDB tayari imeshapata hasara, TIB tayari imeshapata hasara maana yake nini? Maana yake ni kwamba hizo benki projection ya mbele kule miaka miwili, mitatu zinakwenda kufungwa, inakuwa another crisis of Tanzania. Waziri wa Fedha amekaa tu anatazama hali hii! Waheshimiwa Wabunge, mabenki yakifungwa na huku yametoa mkopo businesses hazirudishi mikopo, hebu angalia crisis na tatizo la uchumi wa ndani ya nchi litakavyokuwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema Mheshimiwa Bashe inawezekana hawa hawakwenda kuomba kura hawaelewi joto la wananchi kule.
Sisi ndiyo tunakwenda, ndiyo frontline. Tatizo lingine unaweza kuwa umeteuliwa na Mheshimiwa Rais, basi kule kuteuliwa tu unajiona wewe bora kweli, hapa lazima useme kweli! (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Jimbo la Solwa, tuna ahadi tumeahidi na kesho nina swali hapa tutabanana tu na TAMISEMI, unakwenda unaongea, unadanganya mpaka unachoka, yapo mambo unachoka kudanganya! Ameahidi Kikwete ameondoka, amekuja Pinda ameondoka, anakuja Magufuli ataondoka na baadhi ya miradi haitawezekana kufanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri, fedha ambazo mmezichukua za hizi parastatals companies, haya Mashirika ya Hifadhi ya Jamii mmekwenda kuziweka kabatini BOT, warudishieni wenyewe wazifungulie akaunti kwenye commercial banks, waachie wenyewe iwe ni kama another income of their source. Zile fedha wao watapata, benki zitaendelea kuzitumia ku-lend kwa customers, uchumi kidogo utaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wa pili, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha alipe madeni ya ndani ili fedha zianze kuzunguka sasa hivi kuna joto. Leo Wabunge si mnaona hapa, jana mlikuwa mnaongea sijui nini, hata Bunge hapa ukata mtupu kwa kwenda mbele. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mbunge wa CCM. Tukienda kwenye party caucus tukafanye maamuzi kweli kwa sababu ya nchi yetu na Serikali yetu hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lingine, wakati ule niliwahi kumshauri Waziri wa Fedha nikasema Mawaziri watakuwa wanafanya kazi kwa matukio, unasubiri tukio likitokea unaenda ku-deal nalo kwa sababu hatuna Department ya Research and Development. Tunaweza tukaanzia na Wizara ya Fedha, Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Miundombinu ili research zile zijulikane kwenye sekta ya viwanda na Serikali kwa ujumla wake. Ukiweka juu ya meza unakuja hapa na mpango wako yako mambo ya kubadilisha sheria, ya kurekebisha sera matatizo haya yote yatapungua na wananchi watapata ahueni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Japan mwaka 1980 waliweka 2% ya bajeti yake kwenye R&D yaani unafanya utafiti wa sehemu gani tumekosea, tufanye nini, tuboreshe nini ili uwekezaji ukipita pale uweze kunufaika. Australia 1.5 mwaka 1982 ya bajeti yake na ndiyo iliyowapeleka mpaka leo nchi zile zimeweza kuendelea. Leo unakuja na Mpango umeutoa wapi, umefanya research gani? Tutabaki tunahangaika na tunalalamika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nilikwenda kwenye Kamati ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara walikuja wawekezaji wa nchi nzima, wawakilishi kutoka Bakhresa, Mohammed Enterprises, wafanyabiashara wengi walikuja na kila aliyesimama analalamika, halafu unasema Tanzania ya viwanda, halafu unasema Magufuli ataweza kuleta viwanda, ukiwasikiliza wale wanavyolalamika, ukiona sera na sheria zimepitwa na wakati hatuwezi kufika. Kama ni viwanda kwa style hii hatuwezi kufika kwa sababu kuna mambo ya kurekebisha kwenye viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TIC, One Stop Center, ukienda pale hakuna cha One Stop Center kuna Many Stop Centers, unaweka document yako pale hakuna maamuzi, documents zinachukuliwa zinaenda TRA, TRA pale wiki mbili tatu, mwezi irudi, unangoja certificate umalize pale, maamuzi yanachelewa, kila mtu hana maamuzi. Tatizo ni kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niongelee kuhusu viwanda. Tukitaka tu-win kwenye viwanda sheria lazima ibadilishwe baada ya kufanya utafiti wa kina. Kuna tatizo kubwa sana TBS, kuna tatizo kubwa sana NEMC na siyo kwamba wao ni tatizo, tumechukua sheria za nje, tumezi-copy tukazi-paste kwetu, imekuja kwenda tofauti na uhalisia wa wawekezaji ndani ya nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi hii wawekezaji watakaoweza ku-win vizuri wale wanaotoka nje, wakubwa, anakuja na dola milioni 50, milioni 200, wale ndiyo watakuja kuimeza nchi hii. Mkitaka Watanzania waweze kuinuka kwa sheria tulizokuwa nazo, kwa watendaji ambao wanafanya kazi kwa mazoea bila kuwa na mfumo rasmi, bila kubadilisha mfumo na sera ya nchi nzima, hatuwezi kufika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nikimwambia Mheshimiwa Waziri wa Fedha alete taarifa ya kodi wanazokusanya kuachana na arrears, kama mtu alikuwa ameuza gari nane au kumi, unamwambia bwana kuna gari 10 uliuza lipa hizo hela, sisi tunakutambua wewe kwa sababu hiyo gari ulinunua kwa jina lako na TIN number yako, unabebeshwa mzigo siyo wako. Sasa ile itafika mahali itakwisha, itafika mahali arrears zitakwisha utabaki na cash revenue ya siku hiyo, hapo ndipo utakapoona kutoka 1.5 trilioni inashuka inakuja mpaka kwenye bilioni 800 ambapo Rais Kikwete ameiacha hiyo. Rais Kikwete ameacha bilioni 850 nchi ilikuwa nzuri mambo yanaenda raha kwa kwenda mbele. (Makofi/Vigelegele)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Magufuli ana vision kubwa ya nchi hii anatamani nchi hii itoke tufanane kama Thailand walivyotoka. Hata hivyo, ninavyoona tatizo ni wasaidizi wake ama mnamwogopa au hamumwambii ukweli, mnaogopa kufukuzwa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Magufuli tumefanya naye kazi hapa miaka kumi, mimi nimefanya naye kazi namfahamu, ukienda na data vizuri ukamwambia Mheshimiwa Magufuli kwa tatizo la bandari kuna mambo mawili, mimi nataka niongelee kukimbiwa na wafanyabiashara wa nchi jirani sitaki kuongelea mizigo ya ndani ya nchi, kuna vitu viwili paleā€¦
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukimbiwa na wafanyabiashara kutoka Zaire, jana Mheshimiwa Waziri wa Miundombinu anajibu kana kwamba yeye ni Waziri wa Zaire ndani ya Bunge la nchi hii. Anasema sisi tumeweka ofisi pale ili Wazaire wawe wanalipa ushuru pale kwa sababu wao wanakwepa ushuru inatuhusu nini mambo ya Zaire sisi humu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwawekea ofisi Wazaire walipe ushuru pale ndiyo iliyowakimbiza. Rais Kabila amekuja hapa kwa Magufuli kama alikuwa anataka Wazaire walipie ushuru hapa angeshindwa? Wangeweka sheria pale Bungeni kwamba mizigo yote isipotoka bandari ya Dar es Salaam haingii Zaire lakini yeye ndiyo amewa-encourage akasema nendeni Mombasa, nendeni kule Beira halafu hamuelewi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawaambia bandari yetu inakufa kwa sababu ya mambo manne, naongelea mizigo ya transit siongelei mizigo ya ndani naomba mnielewe hivyo, tunapoteza revenue billions of money. Sababu ya kwanza ni hiyo Single Custom Territory, toa hiyo! Ya pili ni VAT on transit goods. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiongelea kontena moja moja huwezi kuipata kuna meli kama Impala analeta meli tano mpaka sita, akishusha meli yake pale malori 10,000 yanapakia miezi mitatu yanakwenda lakini leo tunamweleza haelewi. Kenya hawana VAT wamesoma sheria zetu, Mozambique wamesoma sheria zetu wameona Watanzania hawa hawaelewi kitu wapo hivi, wao wakaondoa VAT, sisi siku saba tunawapa free wao wameweka siku 90, sijui Single Custom Territory wametoa, check point sisi tunazo sita wao wameweka mbili, tayari wao wamekuwa kwenye advantage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunakosa mapato, hoja hapa tunakosa nini?
Billions of billions zinapotea. Bandari hii ingefanyiwa kazi vizuri ina uwezo wa kuingiza shilingi trilioni tano kwa mwaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Singapore in and out containers milioni 30 kwa mwaka, Dubai milioni 27 sisi 500,000 aibu! Jiografia yetu imekaa vizuri tu, jamani bandari muifanye kama private sector, one of the objective of the business is to make profit, bandari ibadilishwe mfumo ikae pale kama private sector kwa ajili ya kuleta mapato kwa Serikali yetu. Sasa leo Mheshimiwa Waziri wa Fedha anaenda anawabana watu mpaka hawa wenye bodaboda anaenda anawabana anaacha mapato yale, mapato bandarini shilingi trilioni tano anaacha anaenda kubana bodaboda kwa Sh. 50,000 au Sh.100,000 ni nini hii? Waheshimiwa Wabunge tuna vikodi vidogo vidogo vingi sana na ni kero katika nchi hii sasa hivi. Leo hapa traffic wanakamata magari kama kuna vita, ukikamatwa Sh. 30,000, kundi la madereva ni hatari kwenye kura za CCM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamba inaajiri zaidi ya watu milioni 16. Mimi natoka kwenye Mkoa wa Shinyanga, nimeongea nadhani nimeeleweka, Waziri wa Fedha asiponielewa safari hii itakula kwake baadaye. Sisi ni Wabunge wa CCM kule tutafanya maamuzi magumu tu, hatuwezi kuiacha nchi hii inayumba, nchi imeyumba tuseme ukweli. Kwa sababu tukianza kufichaficha hivi tunamficha nani? Sisi ndiyo tunajua 2020 tutashinda, hatuna tatizo lakini lazima sisi wenyewe turekebishe humu! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa pamba leo inaajiri watu milioni 16, mimi natoka kwenye Mkoa wa Shinyanga, tumeongea viwanda, Serikali itafute wawekezaji, sasa hivi Mheshimiwa Magufuli kwa nia njema tu ametaka haya mashirika yetu ya umma yaingie huko, sasa kama kuna mpango huo, niombe mashirika hayo yalete viwanda kwenye Mkoa wa Shinyanga, viwanda vya nguo vikubwa. China na India kiwanda kimoja cha nguo kinanunua pamba yote ya nchi hii, tunataka viwanda vya aina hiyo. Kiwanda kimoja kiweze kununua pamba yote ya nchi hii na kiweze kutengeneza uzi na nguo na ku-add value ili sasa kutengeneza soko la uhakika kwa wakulima wa pamba wa Mkoa wa Shinyanga.